Tuesday 13 February 2018

Conte Awapongeza Mashabiki Chelsea ikishinda 3-0


LONDON, England
KOCHA wa Chelsea Antonio Conte amewapongeza mashabiki wa klabu hiyo kwa kumuunga mkono, baadaya ushindi mnono dhidi ya West Bromwich Albion katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Stamford Bridge na kuounguza presha kwa Muitalia huyo.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya England, Chelsea ambao ni mabingwa watetezi wa England, waliibuka na ushindi wa mabao 3-0.

Hatma ya Conte katika klabu hiyo ya Chelsea iko katika wakati mgumu baada ya timu hiyo kutofanya vizuri msimu huu.

Chelsea ilipokea vipigo vizuri mfululizo kutoka kwa Bournemouth na Watford, lakini ushindi huo wa juzi katika Ligi Kuu kumeirejesha timu hiyo katika mstari wa ushindi.

Jina la Conte lilikuwa likitajwa katika nyimo za mashaiki hao waliokuwa kwenye uwanja wa nyumani, ikiwa ni wazi ilionesha kumuunga mkono kocha huyo.

"nawashuuru mashabiki kwa sababu wameniunga mkono kwa kiasi kikubwa sana, “alisema kocha huyo. “Pamoja na uvumi na tetesi kwangu nina furaha kubwa.”

"Ina maana wamenielewa, nia yangu ya kutetea jezi ya klabu hii na nembo ya klabu hii.”

"Natakiwa kuishi na presha hii hadi mwisho wa msimu. Sitaki shinikizo hili kukaa mabegani mwa wachezaji.”

Ushindi huo umeifanya Chelese au the Blues pointi moja mbele ya Tottenham iliyopo katika nafasi ya tano.

Wakati huohuo, West Brom wako pointi saba kutoka katika ukanda salama katika msimamo wa ligi hiyo baada ya kushinda mchezo mmoja katika mechi 25 walizocheza.

No comments:

Post a Comment