Monday 26 February 2018

Norway Bingwa jumla Olimpiki Majira ya Baridi 2018

PYEONGCHANG, Korea Kusini

NCHI ya Norway imetwaa ubingwa wa jumla wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi huku Marit Bjorgen akishinda medali ya dhahabu kwa mbio za nyika za wanawake za kilometa 30.

Brorgen alitwaa medali hiyo ya dhahabu katika siku ya mwisho ya michezo hiyo iliyofanyika jijini hapa.

Norway imemaliza michezo hiyo ikiwa imejikusanyia jumla ya medali 14 za dhahabu sawa na Ujerumani, lakini imepata medali 39 kwa ujumla, ikiwa n inane zaidi ya Ujerumani.

Bjorgen, 37, amekuwa mchezaji mwenye medali nyingi zaidi katika michezo hiyo ya mwaka huu kwa kushinda medali ya shaba ya timu, ikiwa ni medali yao ya tano katika michezo ya Pyeongchang 2018 na ni ya 15 kwa ujumla.

Mdada huyo alishinda medali katika kila m,chezo alioshindana katika Olimpiki ya mwaka huu.

Pia alishinda medali ya dhahabu ka katika shindano la wanawake la mbio za kupokezana vijiti la 4x5, alipata medali ya fedha katika kilometa 15.

Akishindana katika Olimpiki yake ya mwisho baada ya miaka 16 ya kushiriki michezo, Bjorgen alimaliza akiwa na medal inane za dhahabu, nne za fedha na tatu za shaba kutoka katika michezo mitano.



No comments:

Post a Comment