Wednesday 28 February 2018

Yanga Yavunja Mwiko wa Kutoshinda Mtwara


Na Mwandishi Wetu,Mtwara
MABINWA wa soka Tanzania Bara, Yanga leo imefanikiwa kuvunja mwiko wa kutoibuka na ushindi kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona baaba ya kuibuka na ushidi wa mabao 2-1 dhidi ya Ndanda FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ushindi huo unawafanya mabingwa hao watetezi kufikisha pointi 40 baada ya kucheza mechi 19, wakizidiwa pointi tano na vinara wa Ligi Kuu, Simba wenye pointi 45.

Katika mchezo wa leo uliochezeshwa na refa Florentina Zablon wa Dodoma aliyesaidiwa na Abdallah Rashid na Kassim Safisha wa Pwani, hadi mapumziko tayari Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-0.

ius Charles Buswita ndiye aliyeifungia Yanga bao la kwanza  dakika ya tano akimalizia kazi nzuri ya kiungo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Papy Kabamba Tshishimbi.

Beki wa kulia, Hassan Ramadhani Kessy akaifungia bao la pili Yanga SC dakika ya 29 baada ya kuwalamba chenga mabeki wa Ndanda kufuatia pasi ya Buswita aliye katika msimu wake wa kwanza Jangwani tangu asajiliwe kutoka Mbao FC ya Mwanza.

Yanga ingemaliza kipindi cha kwanza inaongoa kwa mabao 3-0 kama si kiungo Mkongo, Tshishimbi aliyesajiliwa msimu huu kutoka Mbabane Swallows ya Swaziland kukosa penalti dakika ya 38, ambayo ilipanguliwa na kipa Jeremiah Kisubi kufuatia John Tibar George kuunawa mpira kwenye boksi.

Kipindi cha pili, Ndanda walio chini ya kocha Malale Hamsini walibadilika na kuanza kupeleka mashambulizi langoni mwa Yanga hadi kufanikiwa kupata bao la kufutia machozi.

Bao hilo lilifungwa na Nassor Kapama dakika ya 46 akimalizia kazi nzuri ya kiungo Mrisho Khalfan Ngassa, mchezaji wa zamani wa Fanja ya Oman, Free State Stars ya Afrika Kusini, Yanga, Simba, Azam, Azam FC za Dar es Salaam, Mbeya City, Kagera Sugar na Toto Africans ya Mwanza.

Kikosi cha Ndanda FC kilikuwa; Jeremiah Kisubi, William Lucian ‘Gallas’, John Tibar George/Ally Suleiman dk77, Hemedi Khoja, Ahmad Waziri Tajiri/Waziri Majogoro dk40, Jacob Massawe, Majjid Khamis Bakari, Nassor Yahya Kapama, Ahmed Siasa Msumi, Baraka Gamba Majogoro na Mrisho Khalfan Ngassa.

Yanga SC; Youthe Rostand, Hassan Kessy, Mwinyi Mngwali, Kelvin Yondan, Said Juma ‘Makapu’, Raphael Daudi, Pato Ngonyani, Papy Kabamba Tshishimbi/Geoffrey Mwashiuya dk46, Pius Buswita, Ibrahim Ajib na Emmanuel Martin/Yussuf Mhilu dk86.

No comments:

Post a Comment