Tuesday 27 February 2018

Rais Ramaphosa atangaza baraza lake la Mawaziri


JOHANNESBURG, Afrika Kusini

RAIS mpya wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametangaza baraza lake la mawaziri, huku akifanya mabadiliko kadhaa katika nafasi za uwaziri.

Amemteua tena Nhlanhla Nene kuwa Waziri wa Fedha, akibadili uamuzi wa kumtema uliofanywa awali na mtangulizi wake Rais Jacob Zuma.

Bwana Zuma, ambaye anakabiliwa na mashataka ya rushwa, alilazimishwa kuachia ngazi na chama chake mapema mwezi huu.

 Bwana Ramaphosa alichukua madaraka ya urais, aliahidi kupambana na rushwa.

"Nimeamua kufanya mabadiliko haya. Nina hamu ya mabadiliko, kiuchumi na mambo mengine, “alisema Ramaphosa wakati akitangaza uteuzi wake wa mawaziri mjini Pretoria jana usiku.

David Mabuzza, Naibu Waziri wa Chama cha National Congress (ANC) chama tawala, alitangazwa kuwa Naibu Rais wa Afrika Kusini.

Mke wazamani wa Zuma, Nkosazana Dlamini-Zuma, ambaye Ramaphosa alimshinda katika uchaguzi wa Desemba wa ANC, alichaguliwa kuwa waziri katia ofisi ya rais.

Gumzo kubwa lilikuwa kwa Nhlanhla Nene ambaye ameteuliwa kuwa waziri wa fedha, alitimuliwa Desemba mwaka 2015.

Ramaphosa, mwenye umri wa miaka 65 ambaye ni mfanyabiashara wazamai, katika hotuba yake ya kwanza kulihutubia taifa mapema mwezi huu aliahidi kupambana na kuinua uchumi na kutoa ajira.


No comments:

Post a Comment