Monday 26 February 2018

Chelsea wamuongezea dau Hazard ili abaki


LONDON, England

KLABU ya Chelsea ina mshawishi Eden Hazard kuklubali kusaini mkataba mpya kwa kumuongezea daua hadi kufikia pauni 300,000 kwa wiki.

Klabu hiyo ya Stamford Bridge inamshawishi mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji kusaini mkataba mpya na kuzivunja nguvu timu pinzani zinazotaka kumsajili mchezaji huyo.

Pamoja na mchezaji wa Bayern Munich, Robert Lewandowski, Hazard na mchezaji mwenzake Thibaut Courtois ni miongoni mwa wachezaji wanaowindwa na Real Madrid mwaka huu.

Chelsea inataka kuwabakisha wachezaji wake hao wote.

Hazard mwenye umri wa mika 27 mkataba wake wasasa unamalizika mwaka 2020.

Mkataba wake huyo una thamani ya pauni milioni 200 na mkabata wake mpya utamfanya kulipwa pauni 300,000 kwa wiki pamoja na bonasi.

Hazard amekuwa akisema mara kwa mara kuwa ana furaha Chelsea ingawa atakuwa akisubiri kuona kile kitakacholetwa na Real Madrid katika ofa yao.

Kocha wa timu hiyo ya Hispania Zinedine Zidane inamtaka sana Hazard lakini nafasi yake hiyo iko katika tishio msimu huu, lakini itategemea na uamuzi wa nyota huyo.


No comments:

Post a Comment