Tuesday 27 February 2018

Trump Afikiria Uchaguzi 2020, Amtaja Meneja Wake


NEWYORK, Marekani

RAIS wa Marekani Donald Trump amemtaja meneja wa kampeni zake za urais mwaka 2020.

Brad Parscale (pichani kushoto), mtaalam wa mitandao, alifanya kazi katika kampeni za Trump 2016 na alisifiwa sana kwa kutumia mitandao ya kijamii vizuri, jambo linalotajwa kumpa ushindi Trump.

Parscale atatumika katika kampeni za uchaguzi mdogo baadae mwaka huu.

Trump anasema Parscale ni mtu sahihi na amekuwa akifanya kila kitu kwa uhakika wa hali ya juu.

Trump alimshinda Hillary Clinton katika Uchaguzi Mkuu wa Marekani uliofanyika Novemba mwaka 2016 na baadae kuapishwa rasmi Januari 20, 2017.


No comments:

Post a Comment