Tuesday 27 February 2018

Liverpool Inaweza Kuichakaza Timu Yoyote-Mane


LONDON, England

SADIO Mane anasema kuwa Liverpool "inaweza kuifunga timu yoyote duniani " wakati vijana wa Jurgen Klopp wakiifukuzia nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu na kukufuzu kwa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Kimsimamo, Liverpool wako katika nafasi ya tatu, pointi mbili nyuma ya Manchester United baada ya kufungwa mara moja katika mechi 19 zilizopita za Ligi Kuu huku ikiwa katika nafasi nzuri ya kusonga mbele katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kushinda mabao 5-0 dhidi ya Porto katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora.

Kikosi cha Klopp kimefunga mabao 103 katika mashindano yote msimu huu huku safu yake ya ushambuliaji ikiwa na Mane, mabao 31, Salah na Roberto Firmino ,ambao wamekuwa wakizisambaratisha safu za ulinzi za timu pinzani.

"Naweza kuhisi kuwa klabu kwa sasa inakwenda katika muelekeo sahihi, “alisema Mane alipozungumza hivi karibuni.

"Kulikuwa na miaka kibao migumu pale Liverpool lakini mambo hayo huwa yanatoke katika kila klabu duniani.

"Kwa sasa tuko katika njia nzuri, hivyo kila kitu kinawezekana. Tunajua kuwa tunaweza kusema kuwa katika siku zetu tunaweza kuifunga timu yoyote duniani.”

Mshambuliaji huyo wa Senegal alisema ari ya timu kwenye uwanja wa Anfield ni nzuri na kuna kujiamini miongoni mwa wachezaji.

"Kila mchezaji mmoja mmoja wakati wote anafurahia kucheza na mwenzake, “alisema. “Wakati wote tunajaribu kumsaidia kila mmoja na tunacheza kitimu.”


No comments:

Post a Comment