Sunday 11 February 2018

Watakaopisha Upanuzi JNIA kufidiwa Viwanja, Fedha

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa pili kulia) kabla ya kukutana na wakazi wa Kipinguni kwenye Kiwana cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) Terminal One kuhusu fidia ya wakazi hao kupisha upanuzi wa kiwanja cha ndege. Kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala (DAS), Edward Mpogolo. Wa pili kushoto ni Mbunge wa Segerea, Mona Kalua na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA).

 
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imesisisitiza kuwa wananchi wa Kipunguni A na Kipunguni Mashariki, ambao wanatakiwa kuondoka katika maeneo hayo ili kupisha upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), watapatiwa viwanja mahali pengine pamoja na kulipwa fedha, imesisitizwa.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye alipozungumza na baadhi ya wakazi wa maeneo hayo katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa JNIA Terminal  I kuhusu upanuzi wa kiwanja hicho.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela wakati Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye alipozungumza na wakazi wa Kipunguni.
Alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Pombe Magufuli kamwe haina nia ya kuwaumiza wananchi, ambapo watu wenye nyumba maeneo hayo watapatiwa viwanja katika maeneo ya Msongola na kupewa fidia ya fedha.

Alisema kuwa siku zote Serikali ya Magufuli inataka kuhakikisha kila mwananchi anapata haki yake anayostahili na sio kumuumiza.
Baadhi ya wakazi wa Kipinguni A na Kipunguni Mashariki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Atashasta Nditiye alipozungumza nao kuhusu fidia watakapopisha upanuzi wa kiwanja cha ndege.
Alisema kuwa jumla ya wananchi 801 walitakiwa kupewa viwanja na tayari Kampuni ya Tanzania Remix ilishaandaa viwanja 537 kwa ajili ya awamu ya kwanza ya ugawaji viwanja hivyo.

Zoezi hilo kwa miaka mingi lilishindwa kufanyika licha ya Serikali kufanya tathmini, na sasa litafanikiwa baada ya wananchi kurudhika na maelezo ya Nditiye baada ya kusema kuwa hata wale ambao hawakufanyiwa tahmini wakati ule, alimuagiza Naibu Mkurugenzi Mkuu kuhakikisha wanafanyiwa tathmini ili nao wapatiwe viwanja na fedha wanazostahili.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye akizungumza na wakazi wa Kipunguni A na Mashariki kuhusu fidia watakapopisha upanuzi wa kiwanja wa cha Kimataifa cha Ndege cha Julius Nyerere. Kulia ni Katibu Tawala wa Ilala, Edward Mpogolo. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Richard Mayongela. 
Alisema tathmini ya awali ilifanyika mwaka 2013 na kusema kuwa wale watakaovunjiwa nyumba zao watapatiwa viwanja na watafidiwa fedha.

Aidha, Naibu waziri alisema wote waliopewa viwanja baada ya kuvunjiwa Kigilagila, ambao hawakuwa wakazi wa eneo hilo na Kipawa, watanyang’anywa viwanja hivyo na kuchukulia hatua za kisheria.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala (DAS), Edward Mpogolo akizungumza wakati Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye alipozungumza na wakazi wa Kipinguni A na Mashariki kwenye kiwanja wa ndege cha JNIA. 
Alisema hata kama watakuwa wamejnga nyuma, lakini wakabainika kuwa walipewa viwanja wakati hawakuwa wakazi wa maeneo hayo, watapokonywa mara moja na kuchukuliwa hatua.

Alisema kuwa baada ya tahthmini kufanyika muda mrefu, wananchi hao wataongezewa asimilia ya fedha za awali kulingana na miaka iliyopo.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Richard Mayongela alisema kuwa maelekezo yaliyolewa na Naibu waziri atayafanyia kazi na ataunda tume kama alivyoagizwa ili kuhakikisha utekezaji unafanyika kwa ufanisi.

Mayongela alisema kuwa yeye kama mtendaji atahakikisha matatizo yote yaliyojitokexa na tayari mchakato wa kushughulikia tatizo hilo ulianza muda mrefu na ameanza kufanikiwa.
Alimtaka Mbunge wa Segerea, Mona Karia kumuagiza kaimu mkurugenzi huyo mkuu wa TAA kazi yoyote nay eye yuko tayari kuitekeleza ili kuhakikisha wanamaliza matatizo yote.

Alisema tayari viwanja 537 vyenye thamani ya Sh bilioni 3.7 vilishakbidhiwa kwa TAA mwezi uliopita pamoja na kuchelewa,  lakini wameshapata viwanja 700 lakini wanatakiwa kwenda kuvihakiki kama kweli vipo kwa ajili ya kuwapatia wahusika.
Alisema  kuwa tayari wananchi 57 kati ya 59 walishabomoa nujmba zao hadi mwezi uliopita na wamebaki wawili,ambao anategemea nao wakati wowote watavunja nyumba zao na kuondoka eneo hilo.

Alisema wiki hii ataunda kikosi kazi ambacho kitachunguza wale aliopewa viwanja wakati hawakuwa wakazi wa maeneo hayo, ambapo kwa kushirikiana na vyombo vvya dola mkondo wa sharia utachukua nafasi yake.




No comments:

Post a Comment