Saturday 10 February 2018

Mourinho alia Sanchez kuchezewa rafu mbaya


MANCHESTER, England
KOCHA wa Manchester United Jose Mourinho anaamini kuwa anatakiwa kupiga kelele zaidi ili kuwalinda wachezaji wake.

Mourinho hakuwa na furaha kutokana na jinsi Alexis Sanchez alivyopchezewa rafu katika mchezo wa wiki iliyopita uliofanyika kwenye Uwanja wa Old Trafford wakati timu hiyo ikishinda mabao 2-0 dhidi ya Huddersfield Town.

Kocha wa Man City Guardiola alirudia kilio chake kutaka wachezaji walindwe zaidi kufutia kuchezewa vibaya mchezaji wake Leroy Sane na mchezaji wa Cardiff, Joe Bennett na kumfanya mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Ujerumani kuwa nje kwa wiki sita baada ya kuumia kifundo cha mguu.

“Labda kocha wake anataka kulia zaidi, “alisema Mourinho kwa adhabu aliyopewa Sanchez.

Leo Jumapili, Manchester United itakuwa mgeni wa Newcastle United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England utakaofanyika kwenye Uwanja wa St  James' Park.



No comments:

Post a Comment