Tuesday 28 April 2015

Hatimaye wasafirishaji wa dawa za kulevya wauawa Indonesia


Magari ya wagonjwa yakiwa na miili ya watu nane waliuawa kwa kupigwa risasi nchini Indonesia, wakiwemo Waaustralia wawili Andrew Chan na Myuran Sukumaran, yalipopigwa picha yakiwasili katika bandari ya Cilacap kutoka kisiwani ilipo jela walipofungwa watu hao.
 


JARKATA, Indonesia
SERIKALI ya Indonesia usiku wa kuamkia leo imewaua kwa kuwapiga risasi wauzaji nane wa madawa ya kulevya baada ya watu hao kuhukumiwa kifo.

Hukumu hiyo imetekelezwa na kikosi maalum cha kuwapiga wafungwa risasi, licha ya wito kutoka kwa mataifa mbalimbali duniani kutaka watu hao wasinyingwe.

Wafungwa hao walikuwa tisa, lakini kuuawa kwa raia mmoja wa Ufilipino, Mary Jane Veloso, kumecheleweshwa baada ya mwanamke mmoja kujiwasilisha kwa polisi Nchini Ufilipino, akisema kuwa ndiye aliyemhadaa mfungwa huyo mwanamke mwenzake, kupeleka dawa za kulevya Indonesia.
Andrew Chan (kulia), na  Myuran Sukumaran (kushoto) ambao waliuawa usiku wa kuamkia leo.
Aidha, raia wawili wa Australia Andrew Chan, 31, na Myuran Sukumaran, 33, walinyongwa pamoja na wafungwa wengine sita na kikosi hicho maalum cha kuwaua wafungwa.

Raia hao wa Australia ndio walikuwa wa kwanza kuuawa baada yam lo wa usiku.

Inaelezwa kuwa Chan ambaye aliukumiwa kifo mwaka 2005 kwa kupanga mpango huo unaoitwa `Bali Nine heroin smuggling plot aliukumiwa kifo miaka miwili iliyopita.
Waaustralia wawili waliouawa na kikosi maalum cha kuua wafungwa usiku wa kuamkia leo.
Chan,ambaye mapema mwaka huu gerezani, alibatizwa na kuwa Mkristo alisema kuwa, Sandiford muda mfupi kabla hajahamishiwa katika kisiwa hicho cha mauaji, alitubu dhambi zake.

Alisema kuwa: 'Siogopi kufa lakini anahofia kufa taratibu. Naogopa risasi na naogopa kwa kuwa hakitakuwa kifo cha haraka. '
Sandiford alihukumiwa kifo huko Bali tagu alipopatikana na hatia ya kujaribu kusafirisha dawa za kulevya zenye thamani ya pauni Milioni 1.6 za cocaine kupitia uwanja wa ndege wa kisiwani mwaka 2012.

Mwanamke Muindonesia ambaye kifo chake kimeahirishwa alisema kuwa alisafirisha dawa hizo ili kuwalinda watoto zake, ambao usalama wao uliuwa hatarini.

Serikali ya Uingereza ilikataa ombo la kumlipia Sandiford ada ya kisheria kwa ajili ya rufaa yake.

Usiku, yalionekana magari ya wagonjwa yakiwa yamebeba majeneza ya Chan na Sukumaran yakiwasili katika 'kisiwa cha kifo' ambako walipigwa risasi na kuuawa.
Picha tofauti zinaonesha jinsi watu waliokumiwa kifo wanavyoandaliwa hadi kuuawa. Picha namba sita inaeleza kuwa, daktari endapo atathibitisha kuwa mfungwa baada ya kupigwa risasi lakini bado ana dalili ya uhai, basi kamanda wa maaskari hao wauaji anammalizia mfungwa huyo kwa kumpiga risasi kichwani kwa kutumia bastola yake.
Familia ya Chan na Sukumaran ilitoa taarifa kufuatia kuuawa kwa ndugu zao hao.

'Leo tumewapoteza Myuran na Andrew. Watoto wetu, kaka zetu, ' walisema katika taarifa hiyo.

'Miaka kumi tangu walipokamatwa, walifanya kila lililowezekana ili waachiwe, na kuwasaidia wengine, lakini hawakusikilizwa.
Mary Jane Fiesta Veloso (katikati), ambaye kifo chake kiliahirishwa baada ya mwanamke mmoja kujisalimisha nchini Ufilipino, akisema kuwa yeye ndiye aliyemdanganya dada huyo kubeba dawa hizo za kulevya.

No comments:

Post a Comment