Friday 3 April 2015

Bayern Munich, Dortmund kama fainali Jumamosi



MUNICH, Ujerumani
KIPA wa Bayern Munich Manuel Neuer anasema mchezo wa Jumamosi dhidi ya Borussia Dortmund utakuwa kama fainali, licha ya wapinzani wao kuchechemea katika ligi kwa sasa.

Bayern wanaongoza katika msimamo wa ligi hiyo ya Ujerumani wakiwa pointi 10 dhidi ya Wolfsburg, wakati Dortmund wako katika nafasi ya 10, Februari walikuwa wakishikilia mkia.

"Wakati wote timu hizi mbili zinapokutana inakuwa kama fainali, ," alisema Neuer.

Kocha wa Dortmund Jurgen Klopp alisema: "amewekeza kila kitu kwa ajili ya mechi hii."

Kikosi hicho cha Klopp kimemaliza katika nafasi mbili za juu katika misimu minne mfululizo, lakini sasa kinafukuzia nafasi ya kucheza katika Ligi ya Ulaya kufuatia kutofungwa mechi saba baada ya kuwa katika ukanda wa kushuka daraja.

Hatahivyo, Bayern itashuka uwanjani kucheza na mpinzani wake huyo bila ya kuwa na wakali wake kama akina Franck Ribery, Arjen Robben na David Alaba – lakini Klopp bado anahofia makali ya Bayern.

"Bayern watakuwa na Thomas Muller, Mario Gotze na Robert Lewandowski katika safu ya ushambuliaji, " alisema kocha huyo swa Dortmund.
"Hatufiki kuwa tuko katika kiwango sawa kama Bayern. Lakini hatufikirii kama hatuna nafasi.

"Ingawa tuko katika nafasi ya 10, tofauti ya pointi katika msimamo ni kubwa, hayo yamepita tugange yajayo, “alisema.

Nahodha wa Bayern Philipp Lahm anaweza kuanza kwa mara ya kwanza tangu Novemba kutokana na maumivu.

"Hadi sasa nimekuwa nikifanya mazoei kwa wiki nne mfululizo, na hiyo ikiwa na maana niko fiti, " alisema beki huyo wa kutegemewa.

No comments:

Post a Comment