Sunday 19 April 2015

Filbert Bayi alipomuaga binti yake Harriette Mkuza Kibaha

Kivazi alichovaa Bi. Harriette Sanka Bayi wakati wa Send Off yake jana Mkuza Kibaha.
Bi. Herritte Bayi akikata keki huku Baba na Mama yake, Filbert (kushoto) na Anna wakimshuhudia wakati wa sherehe yake ya kumuaga (`Send Off Party), iliyofanyika jana katika ukumbi wa shule za Filbert Bayi Mkuza Kibaha.
Bi. Harriette akimlisha keki baba yake kipenzi wakati wa sherehe ya kumuaga binti huyo jana Mkuza Kibaha.

Bw. Filbert Bayi akimlisha keki binti yake Harriette wakati wa Send Off ya kumuaga binti huyo Mkuza Kibaha jana. Kulia mama yake, Anna Bayi akishuhudia.
Bi. Harriette Bayi akimlisha keki mama yake Anna Bayi wakati wa tafrija ya kumuaga binti huyo (Send Off Party).

Harriette Filbert Bayi (kushoto) akimkaribisha maziwa ya mgando mume wake mtarajiwa Egon Kirschsten wakati wa tafrija ya Send of Party iliyofanyika jana katika ukumbi wa shule za Filbert Bayi Mkuza Kibaha.
Baadhi ya washiriki wa upande wa kiumeni wakishangilia wakati wa Send of Party ya Harriette Filbert Bayi jana Mkuza Kibaha.


Bibi mzaa baba wa Harriette Filbert Bayi akiimba wakati wa sherehe ya kumuaga mjukuu wake iliyofanyika Mkuza Kibaha jana.
Wanamichezo mbalimbali waliohudhuria Send of Party ya Harriette Filbert Bayi jana Kibaha.

Bibi yake Harriette (chini), na mtu mwingine walishindwa kujizuia kulia wakati wa Send of Party ya mjuku wake jana Mkuza Kibaha mkoani Pwani.
Wadau wa Mkuza wakifuatilia kwa makini Send Party ya Bi. Harriette Bayi Mkuza Kibaha jana. Kushoto ni Mhariri wa Michezo wa Tanzania Daima, Tulo Chambo na mwandishi wa Mwananchi, Suleiman Jongo wa Mwananchi.

Bi.Harriette (katikati) akiwa na wazazi wake wakati wa shehere ya kumuaga binti hyo jana Mkuza Kibaha.
Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Suleiman Nyambui akimpongeza Harriette Filbert Bayi wakati wa sherehe ya kumuaga binti huyo iliyofanyika Mkuza Kibaha jana.

Mkurugenzi msaidizi wa Michezo katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Juliana Yassoda akimpongeza Harriette Filbert Bayi wakati wa Send of Party ya binti huyo jana Mkuza Kibaha.
Bi. Harriette Filbert Bayi wakati wa Send Off Party yake jana.
`Kula Baby': Bi. Harriette Filbert Bayi akimlisha mume wake mtarajiwa Egon wakati wa Send Off Party jana usiku.

Kula wangu; ndivyo asemavyo Bw. Egon wakati akimlisha mkewe mtarajiwa Bi. Harriette Bayi wakati wa Send of Party jana Mkuza Kibaha.
Bi. Harriette na mumewe mtarajiwa wakati wa Send Party jana.

Mwanamuziki mahiri wa Bongofleva nchini, Banana Zahir Ally Zorro akiimba kibao cha `Nzela' wakati wa Send Party ya Bi. Harriette Filbert Bayi jana Mkuza Kibaha.

No comments:

Post a Comment