Thursday 30 April 2015

Baba yake Mayweather amponda mpinzani wa mtoto wake


Mayweather alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela mwaka 2012.

NEW YORK, Marekani
MANNY Pacquiao hajawa fiti tangu alipopigwa KO na Juan Manuel Marquez mwaka 2013, anasema baba wa Floyd Mayweather na kocha wa bondia huyo.

Na Mayweather Sr (ambaye ni baba wa bondia huyo) anaamini kuwa mtoto wake atamtwanga tena KO Pacquiao watakapokutna katika pambano lenye utajiri mubwa litakalofanyika Las Vegas Jumapili alfajiri kwa saa za Afrika Mashariki.

"Mara unapigwa kama Pacquiao alipopigwa KO na Marquez, kwa muda mrefu huwezi kupigana sana hadi pale itakapotokea tena, " alisema Mayweather Sr.

Mayweather ameshinda mapambano yake yote 47.
"Pambano hili tayari limeshamalizika. Niamini mimi."
Alipoulizwa anafikiri Pacquiao wakati gali alikuwa katika kiwango cha hali ya juu, Mayweather Sr alijibu: "Wakati alipopigwa na Marquez."

Bondia huyo gwiji wa Mexico (Marquiao) mara mbili alipigwa na Pacquiao na alitoka naye sare mara moja kabla hajamtwanga KO katika raundi ya sita katika pambambano lao la nne la mabondia hao.
Mayweather alimtwanga Marcos Maidana katika pambano lake la mwisho katika ukumbi wa MGM Grand mwaka 2014
Gwigi wa Philippine Pacquiao, bingwa wa uzito sita duniani, tangu wakati hu alishinda mapambano yake matatu, ingawa baadhi ya watu wanasema sio mpiganaji mzuri ukilinganisha na huko nyuma.

Hatahivyo, kocha wa Pacquiao kwa miaka 15, Freddie Roach, alisema bondia wake ana kasi vibaya sana wakati huu akijiandaa na pambano hilo dhidi ya Mayweather, ambaye hajapigwa katika mapambano 47 ya kulipwa.

"Manny anajua kuwa KO ni sehemu ya mchezo wa ngumi, " alisema Roach, kocha bora mara saba wa mwaka. "Ikiwa hautaki kupigwa KO, nenda ukafanye kitu kingine na usicheze ngumi.

"Ilikuwa Ko mbaya zaidi dhidi ya Marquez, alikuwa chini kwa muda mrefu. Nilikuwa na wasiwasi aliporuditena katika gym hakukuwa na mabadiliko.

"Lakini Floyd misuli yake imejengeka zaidi na anapiga ngumi pale anapotaka. Hivyo natarajia atataka kumpiga mapema tena kwa KO.

No comments:

Post a Comment