Saturday 4 April 2015

Basi la wachezaji Fenerbahce lashambuliwa kwa risasi




ISTANBUL, Uturuki
BASI la timu ya Fenerbahce usiku wa kuamkia leo Jumapili lilipigwa risasi baada ya vinara hao wa Ligi Kuu ya Uturuki kuibuka na ushindi wa bao 5-1 dhidi ya Rizespor.

Dereva wa basi hilo alijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini lakini hakuna mchezaji aliyeumia katika shambulizi hilo, ambalo lilitokea wakati timu hiyo ikisafiri kwenda uwanja wa ndege wa Trabzon.

Waziri Mkuu Ahmet Davutoglu alisema kuwa uchunguzi utafanyika ili kubaini watu waliohusika na tukio hilo.

Nayo Shirikisho la Soka la Uturuki lililaani shambulizo hilo na Katibu Mkuu wa klabu hiyo Mahmut Uslu alisema tukio hilo halikuwa sahihi.

"Tulikuja hapa kucheza mchezo, tulikuja hapa kucheza soka, " alisema Uslu.

Abdulcelil Oz, ambaye ni gavana wa Trabzon huko kaskazini-mashariki ya Uturuki, awali alisema basi hilo lilionekana kama lilipigwa na jiwe lakini baadae alitoa taarifa nyingine, akisema kuwa, inaonekana lilipigwa risasi.

"Hali ya sasa inaonekana ilikuwa bunduki," alisema Oz. "Ni mapema mmno kusema lolote kwa sasa, lakini ni aina ya risasi kutoka katika bunduki aina ya."

Kundi kubwa la mashabiki wa Fenerbahce walikuwa wakiisubiri timu hiyo kwenye uwanja wa ndege wa Istanbul kuwapokea wachezaji wao wakirejea kutoka katika mechi hiyo.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, ambaye ni mnazi mkubwa wa Fenerbahce, aliripotiwa akimtaka gavawa wa eneo hilo kufanya uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

Fenerbahce ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo na wameshinda taji hilo mara 19, huku baadhi ya wachezaji wake wazamani kama akina Dirk Kuyt, Raul Meireles na Emre katika kikosi hicho.

Huko Istambuli yaliko maskani ya klabu hiyo ambayo imepanga kileleni katika msimamo wa ligi hiyo baada ya ushindi huo wa Jumamosi, pointi moja mbele ya wapinzani wao wakubwa Galatasaray.


No comments:

Post a Comment