Monday 6 April 2015

caf wajiandaa kumpa kura ya ndio blatter



CAIRO, Misri
WAJUMBE wawili watachaguliwa kama wawakilishi wa bara la Afrika katika Kamati ya utendaji ya Shirikisho la Kimataifa la soka (CAF) Jumanne.

Shirikisho hilo la soka la Afrika linatakiwa kuchagua wawakilishi wake watakaoingia katika jopo la watu wazito 25 wa bodi ya maamuzi ya FIFA.

 Mtunisia Tarek Bouchamaoui na Constant Omari Selemani wa Kongo DRC wanapewa nafasi kubwa ya kuongoza katika kura hizo.
Wawili hao wanaoonekana kumbwaga mjumbe kutoka Ivory Coast Jacques Anouma kutoka katika kamati hiyo aliyoitumikia kwa takribani miaka nane.

Wajumbe kutoka nchi 54 pia wataombwa kuondoa kipengele  cha sheria katika Katiba ya CAF kinachohusu ukumo wa umri ili kuweza kumruhusu rais wa sasa wa shirikisho hilo Issa Hayatou kuendelea kuongoza baada ya kumalizika kwa kipindi chake cha sasa.

Kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya Caf, iongozi waliofikia umri wa miaka 70 wanatakiwa kuachia ngazi, hiyo wanataka kuondoa sheria hiyo ili watu hao waruhusiwe kuendelea kuongoza.

Kitendo hicho kitafungua mlango kwa mzaliwa wa Cameroon- Hayatou, ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 68 na anayeongoza kwa muhula wa saba, kuendelea kuongoza baada ya kumalizika kwa muda wake wasasa mwaka 2017.

Awali, Anouma alikuwa mpinzani mkubwa wa kinyanganyiro cha nafasi hiyo ya uongozi lakini sasa ameungana na Hayatou ambaye wapinzani wake wamepungua nguvu kutokana na siasa za soka.

Rais wa Chama cha Soka cha Algeria Mohamed Raouraoua, ambaye awali alionesha nia ya kutaka kugombea nafasi hiyo ya juu ya CAF, aliondoa jina lake katika uchaguzi huo.

No comments:

Post a Comment