Tuesday 29 August 2017

Suarez uso kwa uso na Messi Uruguay ikiikaribisha Argentina katika mechi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018

MONTEVIDEO, Uruguay
LUIS Suarez keshokutwa Ijumaa atacheza dhidi ya mchezaji mwenzake wa Barcelona Lionel Messi wakati timu hizo za Amerika Kuisni zikisaka nafasi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018.

Uruguay ya Suarez itakuwa mwenyeji wa Argentina anayoichezea Messi katika mchezo huo utakaofanyika Ijumaa.

Huku vinara Brazil wakiwa tayari wameshafuzu kwa fainali hizo za mwakani, macho na masikio sasa yatakuwa kwa timuhizo mbili, ambazo zinasaka nafasi ya kufuzu moja kwa moja katika mbio hizo ndefu za kusaka timu 10 za kufuzu.

Colombia iko katika nafasi ya pili katika msimamo huo ikiwa na pointi 24 wakati Uruguay na Chile tayari zimetwaa nafasi mbili za moja kwa moja za kufuzu zikiwa na pointi 23.

Hiyo ina maana kuwa Argentina iliyopo katika nafasi ya tano itakuwa na kibarua kizito wakati itakaposhika kwenye Uwanja wa Centenario jijini hapa kucheza na wapinzani wake hao wa jadi katika historia ya soka.

Argentina bado inachechemea katika mbio zake hizo za kufuzu, imeshinda mechi sita tu kati ya 14, imeonesha uhai chini ya kocha wake mpya Jorge Sampaoli.

Sampaoli, aliyeongoza ushindi wa Chile katika mashindano ya Copa America 2015, itakuwa imepata nguvu baada ya kuifunga Brazil 1-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika Juni.


Ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya timu dhaifu ya Singapore kumemuongezea nguvu Sampaoli.

No comments:

Post a Comment