Sunday 13 August 2017

Joshua ndiye mwamba Kilifm Marathoni 2017

 
 
Na Mwandishi Wetu, Moshi
Josephat Joshua ndiye mshindi wa mbio za Kilifm International Marathoni 2017 zilizofanyika jana mjini haa kwa uande wa wanaume baada ya kutumia saa 1:04:18 huku Dickson Marwa akimaliza wa pili.

Marwa wiki iliyopita alimaliza wa kwanza katika mbio za Bagamoyo Marathoni.

Kwa upande wa wanawake, Mkenya Shelmith Muruki alimaliza wa kwanza kwa kutumia saa 1:16:13 huku mshindi wa Bagamoyo Marathon kwa wanawake, Angel John alimaliza wa pili kwa kutumia saa 1:18;34 wakati Zakia Mrisho alimaliza wa tatu kwa kutumia saa 1:19:82.
Akizungumza mara baada ya kumaliza mbio hizo, Muruki alisema kuwa zilikuwa nzuri na aliata ushindani mkali kutoka kwa Angel.

Joshua alishinda mbio hizo baada ya kuonesha jitihada kubwa kwa kumpita mshindano wake aliyekuwa akiongoza kwa muda mrefu, Chacha Musinde ambaye alionekana kama ndiye angeibuka na ushindi , lakini aliishia kuwa watatu akipitwa hata na Marwa aliyekuwa katika nafasi la pili la uongozi.

 Mshindi wa kwanza katika mbio za kilometa 21 kwa wanawake na wanaume kila mmoja aliondoka n ash 700,000 huku wa pili wakibeba 500,000 na watatu 300,000 wakati wanne 200,000 na watano 100,000.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira alikuwa mgeni rasmi na alitoa zawadi na kukabidhi medali kwa washindi 10 wa uande wa kike, ambao alitaka mbio hizo kuendeleza jitihada za kuendeleza viaji kwa watoto wadogo ili kuiwaibua akina Filbert Bayi wapya.

No comments:

Post a Comment