Tuesday 29 August 2017

Sharapova aanza kuonesha makali US Open 2017

NEW YORK, Marekani
MARIA Sharapova (pichani) amerejea kwa kishindo katika mashindano makubwa ya tenisi kwa kumtupa nje bingwa namba mbili kwa ubora duniani, Simona Halep katika mashindano ya US Open.

Mrusi huyo alishinda kwa seti 6-4 4-6 6-3 mbele ya mashabiki karibu 24,000 katika mchezo uliofanyika hapa.

Sharapova, 30, alikuwa akicheza mchezo wake wa kwanza wa mashindano makubwa tangu alipokuwa akitumikia adhabu ya kifungo cha miaka 15 ya kupatikana na hatia ya kutumia dawa za kuongeza nguvu.

Bingwa huyo wa mwaka 2006 alihitaji kufuzu ili kupangwa katika ratiba kubwa ya mashindano hayo, ambapo sasa anashikilia nafasi ya 146 kwa ubora.

Sharapova alirejea katika mchezo huo Aprili lakini alikuwa akipambana na maumivu ya nyama za paja, akicheza mara moja tu mwezi Mei, na pia alikataliwa kucheza mashindano ya French Open.
Chama cha Tenisi cha Marekani kimechukua hatua tofauti, baada ya kumpatia Mrusi huyo nafasi katika ratiba kubwa mjini New York, na alitumia nafasi hiyo vizuri.

Hii ni mara ya kwanza kwa Sharapova kucheza mashindano makubwa tangu aliposhindwa na Serena Williams mwaka 2016 katika robo fainali ya mashindano ya Australian Open.

No comments:

Post a Comment