Tuesday 29 August 2017

MultiChoice Yatangaza Neema kwa wateja wa DStv!

Yafyeka Bei za Vifurushi Vyote! Wapenzi wa Kandanda ‘Meno Nje’ 

Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande akizungumza jijini Dar es Salaam leo kuhusu bei mpya za vifurushi.
Na Mwandishi Wetu
PANGA LA BEI LAFYEKA;  DStv Premium kwa 8.15%, DStv Compact Plus kwa 11.02%, DStv Compact kwa 16.11%, DStv Family kwa 9.09% and DStv Access (Bomba) kwa 4.88%

 Katika kuhakikisha kuwa wateja wake wote na watanzania kwa ujumla wanaendelea kufurahia huduma za DStv, Kampuni ya Multichoice Tanzania imetangaza neema kubwa kwa wateja wake kwa kufyeka bei za vifurushi vyake vyote, huku pia ikiboresha maudhui na vipindi katika vifurushi vyake hususan vile vya bei ya chini!
  
Habari hiyo njema imetangazwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande, alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam ambapo amesema bei hizo mpya zitaanza kutumika rasmi Septemba mosi 2017.

“Kumjali na kumsikiliza mteja ni nguzo ya uendeshaji wa biashara yetu. Tumesikia maoni ya wateja wetu na wananchi kwa ujumla kutusihi tuangalie uwezekano wa kupunguza bei, tumechanganua kwa kina na tumeamua kutekeleza matakwa yao, leo hii tumepitisha panga kwenye bei za vifurushi vyetu vyote!” alisema Maharage.
 
Akifafanua kuhusu punguzo hilo, Maharage amesema  kumekuwa na punguzo la hadi asilimia 16, ambalo ni punguzo kubwa sana na litakalowapa ahueni kubwa watumiaji wa DStv. Amezitaja bei mpya kuwa ni;

Bei Mpya za vifurushi vya DStv:

Kifurushi                    Bei ya sasa                     Bei Mpya                % Ya Punguzo
Premium                   TZS 184 000.00            TZS 169 000.00             8.15%
Compact Plus         TZS 122 500.00            TZS 109 000.00                11.02%
Compact                   TZS 82 250.00              TZS 69 000.00               16.11%
Family                        TZS 42 900.00              TZS 39 000.00                9.09%
Access (Bomba)    TZS 19.975.00               TZS 19 000.00                 4.88%

Mara baada ya kutaja bei hizo Maharage aliwaambia waandishi wa habari; “Kwa lugha ya mtaani wanasema ‘Vuma Vimekaza’ – ikimaanisha hali ya kifedha imebana… Multichoice imelisikia hilo na kuamua kuwapa wateja wote wa DSrv ahueni kubwa! Sasa kwa wateja wetu wa DStv, ‘Vyuma vimeachia’”


Maharage amesisitiza kuwa Multichoice itaendelea kuwasikiliza wateja wake na kuhakikisha kuwa inatekeleza kile wanachohitaji wateja wake pale inapowezekana.

“Wateja wetu walituomba tuongeze maudhui ya kitanzania kwenye king’amuzi chetu, tukawasikia, tukaweka chanel maalum kabisa ya Maisha Magic Bongo ambayo ina asilimia 100 ya maudhui ya Kitanzania; wakatuomba tupunguze bei ya vifurushi, tukafanya hivyo mwishoni mwa mwaka jana, na leo tena kwa mara ya pili tumepunguza bei, wakatuomba tuongeze chanel kwenye vifurushi vya bei ndogo, tukafanya hivyo, tukaleta Laliga na Ligi kuu ya uingereza hadi kwenye kifurushi cha chini kabisa cha Bomba”.
 
“Kipekee kabisa Wananchi kupitia serikali wakatuomba tuongeze nguvu kwenye kuinua vipaji vya vijana wetu wa kitanzania, tukasikia, tukaitikia, tukaanza katika riadha ambapo tumemdhamini mwanariadha wetu Alphonce Simbu. Sote tunajua matokeo yake, sasa Tanzania inahofiwa kwenye ulingo wa riadha kimataifa! Haya yote tumefanya kwa sababu tunawasikiliza wateja wetu, tunawasikiliza wadau wetu, tunawasikiliza Watanzania” alisema Maharage.

Wakati habari hii ikiwa ni njema kwa watanzania wote, washabiki na wanazi wa kandanda wameonekana kufurahia Zaidi kwani kwa punguzo hilo kuwa wataweza kushuhudia ligi kuu ya uingereza PL pamaja na ligi nyingine kubwa ulimwenguni na makombe maarufu kama UEFA kwa bei nafuu zaidi.


Kwa maelezo Zaidi kuhusu bei mpya na vipindi mbalimbali katika vifurushi vya DStv tembelea; www.dstv.com.

No comments:

Post a Comment