Friday 25 August 2017

Zanzibar yapongeza TAA kushirikishwa TB III

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, TAA, Salim Msangi akitoa maelezo kwa wajumbe wa  Kamati ya Ardhi, Mawasiliano na Mazingira wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar walipotembea jengo la Terminal 3 la Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA) leo. Kushoto ni mwenyekiti wa kamati hiyo, Hamza Hassan Juma, Naibu Waziri wa Maliasili Mohamed Ahmad Salum na kulia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Juma Makungu Juma.
Na Neema Harrison, TUDARCO
KAMATI ya Ardhi, Mawasiliano na Mazingira ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, imepongeza kushirikishwa kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), katika mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bw. Hamza Hassan Juma alitoa pongezi hizo mara baada ya kutembelea jengo hilo, na kupata maelezo na ufafanuzi mzuri kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa TAA, Bw.. Salim Msangi, ambayo yanaonesha kwa kiasi kikubwa wameshirikishwa.

“Hongereni sana kwani huu mradi ni tofauti kabisa tumeona maelezo yako yanaonesha ni kwa kiasi gani mmeshiriki kuanzia mwanzo wa ujenzi hadi sasa unakaribia kumalizika, ni tofauti nakwetu siku ya mwisho ndio tunakabidhiwa mradi na tunakuwa hatujui chochote zaidi ya kukabidhiwa tu,” amesema Bw. Juma.

Naye Bw. Msangi amesema ndani ya mradi huo kumekuwa na wahandisi wa idara mbalimbali ikiwemo ya umeme walioanza tangu mradi unaanza ili baada ya mradi kukamilika inakuwa rahisi na kutambua eneo litakalokuwa na tatizo kwa ajili ya marekebisho.

Amesema katika ziara hiyo wameweza kujifunza kutoka kwa Wawakilishi hao ikiwa ni njia ya kupeana uzoefu na chachu ya maendeleo katika Viwanja Vya Ndege, ambapo katika jengo hilo kuna mifumo ya ukaguzi wa mizigo hatua tano, na endapo mzigo utakuwa na tatizo unazuiwa kwa ukaguzi zaidi katika hatua ya mwisho.

“Hii mifumo ni ya kisasa zaidi kwani hata kama abiria akiona mzigo alioweka na hauruhusiwi kupita kwenye kiwanja chetu, asidhani atakuwa amesalimika katika hatua ya tano atazuiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,” amesema Bw. Msangi.

Pia amesema jengo hilo litakuwa mitambo maalum utakayowatambua kirahisi abiria watakaokuwa wakisafirisha madawa ya kulevyia wakiwa wameyameza, ambapo awali ilikuwa rahisi kuwatambua kutokana na utaalam walionao maafisa usalama.

Naibu Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji wa Zanzibar, Bw. Mohamed Ahmada Salum amezungumzia kuwa TBIII itatoa ajira kwa wwatanzania wengi .


Bw. Salum amesema JNIA itarajie mashirika mengi ya ndege kujitokeza kwa wingi kufanya safari zake, na zitaongeza pato la taifa.

No comments:

Post a Comment