Tuesday 29 August 2017

Chipukizi amtupa nje bingwa US Open

NEW YORK,Marekani
BINGWA mtetezi wa mashindano ya US Open kwa upande wa wanawake, Angelique Kerber (pichani) ametupwa nje ya mashindano hayo baada ya kuchemcha katika mchezo wa raundi ya kwanza dhidi ya Mjapan Naomi Osaka.

Mjerumani huyo anayeshikilia nafasi ya sita kwa ubora, alijikuta akigalagazwa na chipukizi mwenye umri wa miaka 19 ambaye anashiklilia namba 45 kwa ubora duniani, ambaye alishinda kwa seti 6-3 6-1 kwenye Uwanja wa Arthur Ashe huko Flushing Meadows.

Ni mwendelezo wa mwaka wa shetani kwa Kerber mwenye umri wa miaka 29, ambaye hajashinda taji lolote tangu alipotwaa ushindi jijini New York miezi 12 iliyopita.

"Bado ni mchezaji yule yule na mtu yule yule, “alisema.

"Najua kuwa nina nguvu na najua nitarejea nikiwa na nguvu zaidi, hilo nina uhakika nalo.

"Najua kuwa sitajisalimisha kama hivi. Kwangu, nitajaribu kusahau mechi hii haraka iwezekanavyo na kuangalia mbele tena
ili kupatya mafanikio.”

No comments:

Post a Comment