Sunday 27 August 2017

Mayweather amsimamisha McGregory raundi ya 10

LAS VEGAS, Marekani 
Floyd Mayweather ametimiza pambano la 50 katika ngumi za kulipwa akicheza bila ya kupoteza baada ya kumchapa kwa TKO Conor McGregor katika raundi ya 10 ya pambano hilo.

Mayweather amepata ushindi huo dhidi ya bingwa wa michezo ya UFC (ngumi na mateke).

Mwamuzi alilazimika kuingilia na kusimamisha pambano katika raundi ya 10 baada yya kuona Mayweather anamuangushia kipigo kikali McGregor raia wa Ireland ambaye hakuwa akijibu kitu tena.

Hatahivyo, McGregor amewashangaza wapenda ngumi duniani baada ya kuongoza kuanzia raundi ya kwanza hadi ya tatu.

Kuanzia raundi ya nne, Mayweather alianza kucharuka na taratibu ilipofika raundi ya saba, ilionekana McGregor amepoteza mwelekeo.

Katika raundi ya 8, McGregor alionekana kuchoka hasa miguu, hivyo kutoa nafasi kwa Mayweather kumpiga ngumi nyingi zaidi zilizomfanya achoke zaidi. Huenda angeweza kujitoa katika raundi ya 9 lakini akaamua kuendelea raundi ya 10 ambayo ilimshinda kabisa.

No comments:

Post a Comment