Thursday 10 August 2017

Liverpool yazidi kuigomea ofa ya Barca

LONDON, England
KLABU ya Liverpool imetupilia mbali ofa ya Barcelona ya pauni milioni 90 kwa ajili ya kutaka kumnunua Mbrazil mchezeshaji Philippe Coutinho.

Hiyo ni ofa ya pili kwa Barca kuiwasilisha katika klabu hiyo kwa ajili ya kutaka kumnyakua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambayo ya awali ilikataliwa haraka.

Ofa hiyo ilikuwa ni ya kiasi cha pauni milioni 76 ikongezewa kiasi cha pauni milioni 13.
Hatahivyo, Liverpool imesisitiza kuwa Coutinho, ambaye alijiunga na timu hiyo kutoka Inter Milan kwa ada ua uhamisho ya pauni milioni 8.5, hauzwi.

Barcelona ilimuuza mchezaji wake wa kutegemewa Neymar kwa Paris St-Germain (PSG) kwa rekodi ya ada ya dunia ya kiasi cha pauni milioni 200 wiki iliyopita.

Coutinho aliyefunga mabao 14 msimu uliopita alikaa nje ya uwanja kwa wiki sita akiuguza maumivu ya kifundo cha mguu, alisaini mkataba wa miaka mitano Januari kuendelea kuichezea Barca.

No comments:

Post a Comment