Wednesday 9 August 2017

Naibu Mawaziri wafanya ziara ya mafanikio JNIA

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, TAA, Mtengela Hanga akitoa maelezo mbele ya Naibu Mawaziri watatu walipotembelea Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA) . Hafla hiyo ilifanyikia katika Jengo la Kuwasili na Kundokea Abiria Mashuhuri au VIP.
Na Mwandishi Wetu
NAIBU Mawaziri watatu wamesema kuwa kumalizika kwa Terminal Three ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) kitatatua kero zilizopo Terminal Two.

Kaimu Mkurugenzi JNIA, Johannes Munanka
Hayo yalielezwa jana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lamo Makali wakati akitoa majumuhisho ya ziara yake na wenzake wawili, Hamad Masauni na Edwin Ngonyani wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwenye kiwanja hicho.

Manaibu hao walianza ziara hiyo kwa kutembelea maeneo mbalimbali katika Terminal Two na kukutana na changamoto kibao, zikiwemo kero za msongamano wakati wa hutoaji wa viza kwa abiria wanaowasili.

Kero nyingine ni abiria wanatakiwa kutoka nje ya kiwanja kubadili fedha na kurudi ndani ili kupata huduma katika tawi la benki ya NMB lililopo ndani ya kiwanja hicho ili kulipia viza.

Makani alisema itakapomalizika Termina 3 kero karibu zote zitamalizika kwani jengo la kiwanja hicho linakidhi mahitaji yote muhimu, ambazo ni changamoto katika jengo jingine.

Masauni alisema wizara yake itaongeza askari wa uhamiaji ili kuboresha utendaji kazi kiwanjani hapo, kuongeza idadi ya mashine za viza na kubadilisha mfumo wa utendaji ili kwenda na wakati.

Mhandisi Ngonyani alisema kuwa wanataka kuboresha miundo mbinu, ambapo katika terminal 3 kutakuwa na uboreshaji wa maeneo mengi ili kuwahudumia wasafiri wengi kwa mara moja.

Ngonyani aliishauri Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi kupunguza kutoa viza abiria wanapowasili na badala yake zitolewe katika ofisi za balozi za Tanzania nje ya  nchi kama zifanyavyo nchi zingine ili kupunguza msongamano.
  
Mawaziri hao jana baada ya kumaliza kutembelea JNIA walikwenda katika Bandari ya Dar es Salaam kwa ziara nyingine.


Terminal Three.




Terminal Two.

Msafara wa Naibu Mawaziri walipotembelea JNIA

No comments:

Post a Comment