Tuesday 29 August 2017

Arsena yatupa ofa ya Man City kumsajili Sanchez

LONDON, England
KLABU ya Arsenal imetupilia mbali ofa ya pauni milioni 50 kutoka kwa wapinzani wao wa Ligi Kuu Manchester City kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji Alexis Sanchez (pichani).

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, ambaye alipachika mabao 24 katika Ligi Kuu ya England msimu uliopita, mkataba wake utamalizika katika kipindi kijacho cha majira ya joto na anataka kujiunga na kocha wa City Pep Guardiola.

Arsenal imekuwa ikigoma kumuuza Sanchez, na inataka kumchukua mchezaji wa Man City Raheem Sterling kama sehemu ya mpango huo kabla ya kesho, ambao ni mwisho wa dirisha la usajili.

Lakini Guardiola anajua kuwa anamtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Chile ili kukiimarisha zaidi kikosi chake kwa upande wa ushambuliaji.

Sterling ambaye mwenye umri wa miaka 22, ambaye ni mshambuliaji wa England alipangwa katika mechi zote tatu za Man City za ufunguzi wa Ligi Kuu ya England msimu huu.

Hatahivyo hajahakikishiwa namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza katika timu hiyi yenye maskani yake kwenye Uwanja wa Etihad baada ya kuwasili kwa Bernardo Silva kutoka Monaco.

No comments:

Post a Comment