Saturday 16 September 2017

Ismail Juma avunja rekodi ya nusu marathoni

Na Mwandishi Wetu
Mwanariadha Ismail Juma (pichani) leo Jumamosi ameweka rekodi mpya ya taifa ya Tanzania ya mbio za kilometa 21 au nusu marathoni.

Mtanzania huyo aliweka rekodi hiyo mpya ya taifa kwa kukimbia kwa muda wa dakika 59:30 katika mbio zilizofanyika Jijini Mattoni, Jamhuri ya Czech.

Rekosi ya zamani ya taifa ya dakika 59:52 ilikuwa ikishikiliwa na Dickson Marwa aliyoiweka Februari mwaka 2008 Abu Dhabi, Falme za Kiarabu.

Mshindi wa kwanza wa mbio hizo ni Barselius Kipyego wakati mshindi wa pili ni Josphat Tanui wote wa Kenya.

No comments:

Post a Comment