Sunday 17 September 2017

Mourinho aeleza siri United kumsajili Lukaku

LONDON, England
KOCHA Jose Mourinho anaamini Manchester United ilimsajili Romelu Lukaku kwa sababu kwameweza  kulipa fedha kiasi cha fedha kilichotakiwa na Everton.

Man United walilipa kiasi cha fedha ambacho kinaweza kuongezeka hadi pauni milioni 90 kswa ajili ya kumsajili mshambuliaji huyo wa Ubelgiji,ambaye leo anatarajia kupangwa katika mchezo wa Super Sunday dhidi ya Everton.

Lukaku mwanzo wake wa kucheza Old Trafford ulianza kiaina, ambapo alifunga mabao sita katika mechi sita, wakati mshambuliaji mwingine alikuwa katika mawindo ya United, lvaro Morata, alifunga mabao matatu katika mechi nne za Ligi Kuu ya England akiwa na Chelsea.

The Blues (Chelsea) walilipa kiasi cha auni milioni 6 kwa ajili ya kupata huduma ya Morata na Mourinho anahisi ni suala la fedha tu wakati linaokuja suala la mipango ya kumsajili mshambuliaji huyo, ambao klabu hiyo ilikua na kile muhimu kulipa kwa ajili ya kumsajili Lukaku.

"Sifikiri ni sababu ya ushawishi wangu, hapana, " alisema Mourinho. "Nafikiri tulilipa fedha zilizoombwa na Everton kwa ajili ya mchezaji huyo na mshahara ambao wakala wake aliuhitaji na tulimpa wakala kamisheni aliyoitaka.

"Nafikiri hiyo ndio ilikuwa sababu kubwa. Sioni sababu nyingine. Tulilia kile ambacho Everton walikuwa wakihitaji. Klabu inayomuuza mchezaji ndio inaamua kiasi cha fedha ambacho klabu inayomtaka mchezaji inatatakiwa kulia au kutoliap.

No comments:

Post a Comment