Tuesday 19 September 2017

Kongamano la Kwanza Kitaifa la Usafiri wa Anga lafunguliwa Dar leo na Waziri Mbarawa

  1. Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka leo akifuatilia mada kwenye Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga, linalofanyika kwa siku mbili kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa akiongea na Balozi wa Ufaransa nchini, Bi. Malika Berak mara baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere katika Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga lililoanza leo.

Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka (wa pili kushoto), akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kwa wananchi waliotembelea meza ya maonesho ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), yanayokwenda sambamba na Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga linalofanyika kwa siku mbili kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Prosper Tesha  (kulia) akiwa na Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT), Prof. Zacharia Magnilwa  (katikati), wakimsikiliza Mhandisi Kedrick Chawe, kwenye  maonesho yanayokwenda sambamba na Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga yanayofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (mwenye tai nyekundu waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Kwanza la Usafiri wa Anga linalofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Kushoto kwa Waziri  ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Salim Msangi na kulia Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Bw. Hamza Johari.  

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA),  Bw. Salim Msangi (mbele) leo akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Shirika la ndege Tanzania (ATCL), Mhandisi Ladislaus Matindi (hayupo pichani)  aliyekuwa akiwasilisha mada kwenye Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga, lililoanza leo kwenye  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

No comments:

Post a Comment