Saturday 16 September 2017

Manchester City yaikandamiza Watford mabao 6-0

LONDON, England

SERGIO Aguero amefunga mabao matatu au `hat-trick’ wakati Manchester City ikishika usukani wa msimamo wa Ligi Kuu ya England leo baada ya kutoa kichapo kikali cha  mabao 6-0 kwa Watford.

Awali, Watford ambao ilikuwa haijafungwa nayo pia ingeweza kuongoza msimamo wa ligi hiyo endapo ingekifunga kikosi cha kocha Pep Guardiola, lakini kilishindwa kufanya hivyo.

Kikosi cha Man City sasa kimeshinda mechi tatu na kufunga jumla ya mabao 15.

Watford baada ya kipigo hicho imebaki na pointi zake nane na kuangukia katika nafasi ya 10 ya msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha jumla ya timu 20.

Katika mechi zingine leo; Crystal Palace ilipokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Southampton, huku Huddersfield Town ikitoka sare ya 1-1 na Leicester City na Liverpool ilibanwa na Burnley kwa sare ya 1-1.

Mechi nyingine leo, Newcastle United iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Stoke City, West Bromwich Albion ilitoka suluhu na West Ham United.

Wakati huohuo, Chelsea kesho itacheza na Arsenal wakati Manchester United watakwaana na Everton kwenye Uwanja wa Old Trafford.


MSIMAMO LIGI KUU ENGLAND

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Manchester City54101621413
2Manchester United43101221010
3Chelsea43018539
4Newcastle United53026429
5Huddersfield Town52215328
6Burnley52216518
7Liverpool52219908
8Southampton52214408
9West Bromwich Albion52214408
10Watford522179-28
11Tottenham Hotspur42117347
12Arsenal420278-16
13Stoke City512256-15
14Leicester City511379-24
15Brighton & Hove Albion511347-34
16Swansea City411225-34
17Everton411226-44
18West Ham United5113410-64
19AFC Bournemouth510439-63
20Crystal Palace500508-80

No comments:

Post a Comment