Saturday 9 September 2017

Uchukuzi, Takukuru zilivyochuana katika michezo tofauti

Kikosi cha timu ya soka ya Klabu ya Uchukuzi kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mechi ya kirafiki na Takukuru iliyofanyika kwenye viwanja vya michezo pembezoni mwa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) hivi karibuni, ikiwa ni moja ya maandalizi ya michezo ya Shimiwi iliyokuwa ianze Septemba 15 mkoani Morogoro, lakini imefutwa ili kuelekeza nguvu katika ujenzi wa viwanda. 
 Kikosi cha Takukuru wakiwa kwenye picha ya pamoja kabla ya mechi ya kirafiki dhidi ya Uchukuzi walikuwa wakijiandaa na michezo ya Shimiwi iliyokuwa imepangwa kuanza Septemba 15 mkoani Morogoro, lakini sasa imefutwa na wachezaji kutakiwa kuelekeza nguvu kwenye ujenzi wa viwanda.
timu ya Kamba ya wanawake ya Klabu ya Uchukuzi wakivutana na wenzao wa Takukuru katika mchezo wa kirafiki. Uchukuzi ilishinda mivuto 2-0.


timu ya kamba ya wanawake ya Takukuru wakivutana na wenzao wa Uchukuzi katika mchezo wa kirafiki uliokuwa moja ya maandalizi ya michezo ya Shimiwi, iliyokuwa ianze Septemba 15 mkoani Morogoro, lakini imefutwa. 

Timu ya wanaume ya kamba wakivuta na wenzao wa Takukuru katika mchezo wa yaliyokuwa mashindano ya Shimiwi yaliyokuwa yamepangwa kuanza Septemba 15 mkoani Morogoro, lakini yamefutwa kwa lengo la kuelekezwa nguvu katika ujenzi wa Viwanda.


Timu ya wanaume ya Takukuru wakivutana na wenzao wa Uchukuzi katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu wa maandalizi ya yaliyokuwa mashindano ya Shimiwi yaliyokuwa yamepangwa kuanza Septemba 15 lakini yamefutwa ili kuelekeza nguvu kwenye ujenzi wa viwanda.
Mshambuliaji Charles Rungwa wa timu ya Takukuru akiwatoka wachezaji wa Uchukuzi katika mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na yaliyokuwa mashindano ya Shimiwi yaliyokuwa yamepangwa kufanyika mkoani Morogoro kuanzia Septemba 15, lakini sasa yamefutwa kwa lengo la wachezaji kuongeza nguvu katika ujenzi wa viwanda. Uchukuzi ilishinda magoli 2-1.  

No comments:

Post a Comment