Tuesday 12 September 2017

Kocha Rodgers akikosoa kikosi chake kwa kichapo

LONDON, England

KOCHA Brendan Rodgers anasema kuwa kikosi chake cha Celtic kilicheza kama vitoto vyenye umri chini ya miaka 12 katika kipindi cha kwanza katika mchezo waliofungwa 5-0 na Paris St-Germain (PSG) wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Mabingwa hao wa Scotland tayari walikuwa nyuma kwa mabao 3-0 hadi kipindi cha kwanza kinamalizika katika mchezo huo wa ufunguzi wa Kundi B.

Rodgers alisema hakutaka kuwa mkosoaji mkubwa kwa wachezaji wake lakini walicheza vibaya katika kipindi cha kwanza.

"Unatakiwa kuangalia mpira na unatakiwa kukusaidia, kipindi cha kwanza, hatukufanya hivyo, tulicheza kama watoto wenye umri chini ya miaka 12 wakati huo, “alisema Rodgers.

No comments:

Post a Comment