Tuesday 19 September 2017

Messi atupia manne Barca ikishinda 6-1

BARCELONA, Hispania

LIONEL Messi ameongeza mabao manne katika akaunti yake aliyofunga mapema msimu huu wakati Barcelona ikiendeleza kwa asilimia 100 rekodi yake ya ushindi katika Ligi Kuu ya Hispania ya La Liga baada ya kuifunga Eibar 6-1 jana.

Paulinho na Denis Suarez nao pia walizifumania nyavu katia mchezo wa pili mfululizo wakati Barca ikizidi kujitanua kileleni katika ,simamo wa ligi hiyo hadi kufikia pointi saba zaidi dhidi ya wapinzani wao wakubwa, Real Madrid, ambayo leo watakuwa wenyeji wa Real Betis.

Mapema, Valencia ilipanda hadi katika nafasi ya tatu wakati Simone Zaza alipofunga mabao matatu `hat-tric’ ndani ya dakika saba wakati timu hiyo ikiisambaratisha Malaga kwa mabao 5-0.

Kocha wa Barca Ernesto Valverde alikibalisha sana kikosi chake kwa mara ya kwanza tanbgu alipoanza kuifundisha timu hiyo, ambapo alibadili wachezaji sita kutoka katika kikosi kilichocheza Jumamosi na kushinda 2-1 dhidi ya Getafe.


Messi alianza kufungua akaunti ya mabao katika mchezo huo baada ya kufunga kwa penalti katika dakika ya 21 baada ya Nelson Semedo kuchezewa vibaya  na Alejandro Galvez.

MSIMAMO LA LIGA:


PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Barcelona55001721515
2Sevilla431061510
3Valencia52309369
4Real Sociedad430111749
5Real Madrid42209458
6Atlético Madrid42208358
7Athletic Club42113127
8Villarreal42026516
9Levante41305416
10Leganés42023306
11Las Palmas420257-26
12Real Betis420257-26
13Eibar5203310-76
14Getafe411234-14
15Girona411235-24
16Espanyol411238-54
17Celta de Vigo410357-23
18Deportivo La Coruña4013511-61
19Deportivo Alavés400407-70
20Málaga5005111-100

No comments:

Post a Comment