Monday 3 August 2015

Shule ya Hazina ilipoibuka kidedea katika mtihani wa utamilifu mkoa wa Dar es Salaam kwa mwaka 2015



Wanafunzi wa shule ya msingi Hazina walioshika nafasi ya kwanza hadi ya 10 katika mtihani wa utamilifu mkoa wa Dar es Salaam kwa mwaka 2015 wakiwa katika picha ya pamoja na walimu wao baada ya kutangazwa washindi jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
SHULE ya msingi ya Hazina imeshika nafasi ya kwanza katika mkoa wa Dar es Salaam katika mtihani wa utamilifu wa darasa la saba uliofanyika Juni 4 na 5 mwaka huu.

Ofisa Elimu mkoa wa Dar es Salaam Raymond Komba aliipongeza shule hiyo, ambayo pia ilitoa mwanafunzi wa kwanza hadi wa 10 katika mtihani hiyo.

Majengo ya shule ya Msingi Hazina yaliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam, ambako wanafunzi walioshika nafasi 10 katika mtihani wa Utamilifu na kuzipita shule zote za mkoa huo.
Komba aliyasema hayo katika kikao cha watendaji wa elimu mkoa wa Dar es Salaam, walimu wakuu, wazazi na baadhi ya wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani huo wa majaribio.

Aliipongeza shule ya Hazina kwa kushika nafasi ya kwanza kimkoa katika matokeo yote yaliyojumuisha shule za binafsi pamoja na zile za serikali, huku wanafunzi wake wakishika nafasi ya kwanza hadi ya 10.
Usafiri sio tatizo katika shule ya Hazina, Hilo ni moja ya mabasi ya shule hiyo ambayo hufanya wanafunzi kutohangaika katika usafiri.
 Wanafunzi wa shule hiyo walioshika nafasi ya kwanza hadi ya 10 ni Rajabu Said, Atif Mustifa, Zauditu Ally, Baraka Juma, Tatiana Ally, Warda Agapiti, Witness Jonas Mallosa, Henry Flowin Madiwa, Henry Godfrey Msuya na Ismail Khaliphan.

Jumla ya wanafunzi 58,489 kati ya 59,709 waliosajiliwa walifanya mtihani huo kwa mkoa wa Dar es Salaam, huku shule ya Kijitonyama Kisiwani ikiibuka ya kwanza kwa upande wa shule za serikali pekee.
Mapunda alisema kuwa ufaulu wa kila shule ndio unaotafsiri ufaulu wa wilaya na kuamua ufaulu wa Manispaa kwa ujumla, hivyo alizitaka shule kungeza juhudi wakati wa kuelekea katika mtihani wa taifa wa darasa la saba utakaofanyika Septemba 9-10.

Pia, ofisa huyo elimu alizipogeza shule za mkoa wa Dar es Salaam kwa kushika nafasi ya kwanza katika mtihani wa taifa mwaka jana na kuwataka kufanya vizuri zaidi mwaka huu ili kuendelea kuishikilia nafasi hiyo.

Akizungumza na gazeti hili mwanafunzi aliyeshika nafasi ya kwanza Rajabu Said alisema kuwa wamefanya vizuri kutokana na jitihada za bila kuchoka za walimu wao pamoja na wao kuwa wasikivu na kuelewa kile wanachofundishwa.

Pia, aliahidi shule yao kuendelea kuibuka ya kwanza katika mtihani wa kitaifa utakaofanyika mwezi ujao.




 

Mwanafunzi aliyefanya vizuri zaidi katika mtihani huo kwa kushika nafasi ya kwanza, Rajabu Said akihojiwa baada ya kutangazwa mshindi.
Rajabu Said akipongezwa na Ofisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Komba.

No comments:

Post a Comment