Saturday 8 August 2015

Floyd Mayweather aishi vituko abeba mamilioni ya dola katika mfuko kwa ajili ya maandalizi ya pambano lake la mwezi ujao

Bondia Floyd Mayweather akiweka dolali katika mfuko kwa ajili ya kulipia bili mbalimbali atakapokuwa kambini akijiandaa na pambano lake la mwezi ujao huko Las Vergas.Marekani.

Mwandishi Wetu na Mashirika
BONDIA Floyd Mayweather ameanza maandalizi ya kujiandaa kuchapana na Andre berto Las Vegas mwezi ujao huku akibeba mamilioni ya doa za Marekani kwa ajili ya maandalizi hayo.

Mayweather ambaye hajawahi kupigwa na ndiye anayeshikilia mataji ya WBC na WBA, aliweka katika mfuko mamilioni ya dola kwa ajili ya kulipia gharama mbalimbali atakapokuwa huko akijiandaa kwa pambano hilo.

No comments:

Post a Comment