Friday 2 March 2018

Waziri Mwakyembe Akunwa na Uwekezaji wa Bayi

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (wa pili kulia) akipita mbel;e ya Uwanja wa Ndani wa Michezo wa Filbert Bayi Sports Complex alipotembelea jana baada ya kufungua semina ya kuwawezesha wanawake ndani na kupitia michezo jana Mkuza, Kibaha mkoani Pwani.
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amepongeza uwekezaji mkubwa wa miuondo mbinu ya michezo uliofanywa na mwanariadha wazamani nchini Filbert Bayi.
Dk Mwakyembe aliyasema hayo jana alipotembelea maeneo mbalimbali ya Taasisi ya Fibert Bayi (FBF) yaliyopo Mkuza, Kibaha, ambako kuna viwanja mbalimbali vya michezo vikiwemo viwanja vya nje na ndani.

Mwakayembe baada ya kufungua semina ya kuwawezesha wanawake kupitia michezo iliyofanyika Mkuza, alitembelea maeneo hayo ya FBF na kushuhudia uwanja mkubwa wa ndani wenye viwango vya kimataifa.

Sehemu ya uwanja huo kwa sasa inatumiwa na wachezaji wa timu ya taifa ya mpira wa meza ya Tanzania itakayoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Gold Coast, Australia mwezi ujao.

Dk Mwakyembe alisema kuwa hajawahi kufika Mkuza na wala hakujua kama kuna uwekezaji mkubwa kama huo uliofanywa na Bayi, ambapo aliwataka akina Mbana Samatta kuiga uwekezaji wa uliofanywa ma Bayi.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Filbert Bayi (FBF), Filbert Bayi akitoa maelezo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe alipotembelea taasisi hiyo jana Mkuza, Kibaha. Mwingine pichani ni Mkurugenzi wa shule za Filbert Bayi, Anna Bayi.
Alisema kuwa wachezaji wengi wakipata fedha zaoe wamekuwa wakinunua magari ya kifahari badala ya kuwekeza katika miundo mbinu mbalimbali kama alivyofanya Bayi na kutengeneza ajira kwa watu kibao.

Mbali na uwanja huo wa ndani ambao una viwanja vvya michezo yote ya ndani, pia kuna viwanja vya nje vya soka, netiboli na mpira wa kikapu.
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe akiwa na mmoja wa wakufunzi wa semina ya kuwawezesha wanawake ndani na kupitia michezo aliyofungua jana Mkuza, Kibaha mkoani Pwani.





Daktari Mkuu wa Kituo cha Afya cha Filbert Bayi akisalimiana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe. Wengeni ni Bayi (wa pili kushoto) na mkurugenzi wa Shule za Filbert Bayi, Anna Bayi.

Ukumbi mkubwa wa shughuli mbalimbali wa FBF Mkuza, Kibaha.
Waziri huyo pia alitembelea majengo ya shule ya FBF kuanzia chekechea hadi sekondari, vyumba vya komputa, kituo cha afya, ukumbi na wodi ya wazazi na ile ya wagonjwa wa kawaida.

No comments:

Post a Comment