Sunday 4 March 2018

Wakenya Waendelea Kutamba Kili Marathon

Wanariadha wakichuana katika mbio za Tigo Kili Nusu Marathon leo mjini Moshi.
Na Mwandishi Wetu, Moshi
WAKENYA wameendelea kutamba katika mbio za Kilimanjaro Marathon kwa kilometa 21 na zile za kilometa 42 zilizofanyika leo mjini hapa na kushuhudiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe.

Katika mbio za kilometa 42, Wakenya wameshikilia nafasi 10 za kwanza kwa uoande wa wanaume na wanawake huku Failuna Abdil akiwa Mtanzania pekee aliyekuwemo katika nafasi tatu bora kwa upande wa wanawake katika mbio za kilometa 21 baada ya kushika nafasi ya pili kwa kutumia saa 01:13:52.

Waziri wa Habari,Utanaduni, Sanaa na Nichezo, Dk Harrison Mwakyembe amesema kuwa amesononeshwa a matokeo ya mbio za Kilimanjaro Marathon baada ya Tanzaniaa mmoja tu kuwemo katika tatu bora kati ya washindi 20.

Katika mbio za kilometa 21, Failuna Abdi alimaliza wa pili nyuma ya Mkenya Flavious Kwamboka huku nafasi zingine zote katika 10 bora zikichukuliwa na Wakenya ambao walitawala pia mbio za wanaume za kilometa 21 kuanzia nafasi ya kwanza hadi 10.

Mbali na mbio hizo za kilometa 21, Wakenya pia walishika nafasi 10 za kwanza kwa upande wa wanajume na wanawake katika mbio za kilometa 42 zilizoanzia na kumalizikia kwenye Uwanja wa Ushirika mjini hapa.

Mwakyembe akizungumza baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mbio hizo kwenye uwanja huo alisema kuwa lazima aseme ukweli na hayuko tayari kuwapaka mafuta wakati matokeo hayajamfurahisha baada ya nafasi zote za juu kuchukuliwa na Wakenya.

Aliwataja vijana wa Moshi kufanya mazoezi kwa bidii ili mwakani waweze  kulitoa taifa kimasomaso kwa kufanya vizuri katika mbio hizo na kutwaa fedha zote zinatolewa kwa washindi.

Mwakyembe alipongeza maandalizi mazuri ya mbio hizo ambazo ni kubwa kabisa nchini kwa upoande wa marathon.

Grace Kimanzi wa Kenya alimaliza wa kwanza katika mbio za kilometa 21 kwa kutumia saa 01:13:46 huku Failuna akitumia saa 01:13:52 huku mshindi wa pili tatu ni Mkenya Pauline Rkahenya aliyetumia saa 01:13:54 wakati kwa wanaume, Geofry Torotich wa Kenya alishinda mbio hizo kwa wanaume kwa kutumia saa 01:03:26 na Simon Muthon alikuwa wa pili kwa saa 01:03:29.

Mshindi wa tatu katika mbio za kilometa 21 kwa wanaume alikuwa Shadrack Korir aliyetumia saa 01:03:35, ambao walizawadia sh mil 2, mil 1 na 650,000 kwa upande wa wanawake na wanaume.

Katika mbio za kilometa 42, Cosmas Muteti alimaliza wa kwanza katika mbio hizo kwa kutumia saa 02:17:01, huku mshindi wa pili alikuwa Eikana Yego aliyetumia saa 02:19:25 na George Onyancha aliyetumia saa 02:20:25.

Mwaka huu jumla ya washiriki wa mbio zote za kilometa 21, 42 na zile za kujifurahisha za kilometa tano,walikuwa zaidi 11,000.


No comments:

Post a Comment