Tuesday 13 March 2018

MultChoice Yazindua Tuzo za AMVCA 2018

Mkurugenzi Mkuu wa MultiChoice, Maharage Chande.

Na Mwandishi Wetu
WASANII wa Tanzania wametakiwa kuwasilisha kazi zao kuanzia sasa hadi Aprili 30 kwa ajili ya kushindania tuzo maarufu ya AMVCA 2018.

Mkurugenzi Mkuu wa MultiChoice, Maharage Chande alisema jana, tuzo hizo za Africa Magic Viewers (AMVCAs)wasanii wa filamu wanatakiwa kuwasilisha kazi zao kwa ajili ya kushindanishwa.

Chande alisema kuwa tuzo hizo, ambazo hufanyika kila mwaka zimekuwa zikihusisha maelfu ya wasanii wa filamu kushindana.

Alisema kuwa tuzo zilibuniwa ili kuthamini na kutambua mchango wa watengeneza filamu wa Afrika, waigizaji, waigizaji na wataalam wa sekta ya filamu na telvisheni barani Afrika.

Alisema kuwa tuzo za mwaka huu zinatarajia kuwa kubwa zaidi na ushindani unatarajia kuwa wa aina yake kutoka kwa wasanii mbalimbali.

Alisema kuwa baada ya kimya cha muda mrefu,
Africa Magic ikishirikiana na MultiChoice, hatimaye wametangaza rasmi kuanza kwa kinyanganyiro cha moja ya tuzo maarufu duniani katika tasnia ya sanaa ya filamu.

Tuzo hizo ambazo hufanyika kila mwaka zimekuwa zikihusisha mamia ya washiriki kutoka kila kona ya bara la Afrika na zimekuwa moja ya tuzo zilizojizolea umaarufu mkubwa barani Afrika na duniani kwa ujumla na limekuwa ni jukwaa muhimu la kutambua na kuenzi vipaji vya tasnia ya filamu katika bara la Afrika.

Baada ya mapumziko mafupi, tunayo furaha kutangaza kwamba  mwaka 2018 utakuwa na toleo la mwaka wa sita mfululizo wa MultiChoice na Africa Magic kuandaa AMVCAs kwa mafanikio na tunaendelea kujivunia mabadiliko yanayoonekana kwenye nyanja ya filamu tangu Tuzo zilipoanzishwa.

Katika msimu uliopita, Filamu za Kitanzania ziliwika katika Kundi la Filamu Bora Afrika Mashariki, ambapo Aisha ya  Amil Shivji, Naomba Niseme ya Staford  Kihore, na Homecoming ya Seko Shamte zilichaguliwa huku  Siri ya Mtungi ikijitokeza kwenye Kundi la Filamu Bora za lugha ya Kiswahili.

Msimu uliopita, filamu ya Kitendawili ya Richard Mtambalike ilinyakua tuzo ya filamu bora ya lugha ya Kiswahili wakati Elizabeth Michael Lulu alivuma katika tuzo hizo katika filamu yake ya Mapenzi iliyoteuliwa kuwa filamu bora kabisa Afrika Mashariki.
Kwa maelezo zaidi juu ya mahitaji ya kujiunga na taratibu za uwasilishaji, tafadhali ingia www.dstv.com.


Kuingia AMVCAs ni bure na tarehe ya kufungwa kwa maingizo ni 30 Aprili 2018. Filamu au sinema zilizotayarishwa kwa ajili ya televisheni au tamthiliya za kwenye televisheni ambazo ziliingizwa mwanzoni au kuteuliwa kwa ajili ya tuzo, au kutuzwa zawadi katika shindano lingine la filamu na televisheni zinaruhusiwa kuingizwa kwenye AMVCAs kama zinarushwa au kuoneshwa katika kipindi cha kuanzia Oktoba, 2016 hadi Machi, 2018.

Maelekezo ya kushiriki:

HATUA YA 1

Prepare a 2 to 3 minute long showreel for your online submission. /Andaa ufupisho wa filamu yako wenye muda wakati ya dakika 2 hadi 3 kwa ajili ya kuuwasilisha kwa njia ya mtandao.

HATUA YA 2

Ingia www.africamagic.tv na uende kwenye ukurasa wa kuwasilisha.

HATUA YA 3
Jaza fomu za uwasilishaji na upandishe video yako. Namba ya kipekee ya utambulisho itatolewa kwa kila ingizo la mtandaoni lililokamilika. Kisha kutegemea na eneo ulipo, tuma ingizo lake akionesha namba zake za utambulisho.

No comments:

Post a Comment