Tuesday 20 March 2018

Mtoto wa George Weah Aitwa Kikosi cha Marekani


PARIS, Ufaransa
CHIPUKIZI mshambuliaji wa Paris Saint-Germain (PSG) Tim Weah, mtoto wa Rais wa Libelia na mchezaji bora wa dunia wa mwaka 1995 George Weah, ndiye mchezaji ndogo zai kuitwa katika kikosi hicho kwa ajili ya mchezo dhidi ya Paraguay.

Kocha wa muda wa timu ya taifa ya Marekani Dave Sarachan alitangaza orodha ya wachezaji kwa ajili ya mechi ya kimataifa ya kirafiki Machi 27 itakayofanyika Cary,

Kaskazini ya Carolina, ambayo itashirikisha wachezaji 17 kati ya 22 wenye umri wa miaka 24 au chini ya hapo.

Weah, 18, anajiunga kwa mara ya kwanza katika klabu hiyo ya timu ya taifa ya Marekani baada ya kukichezea mara mbili kikosi cha kwanza cha PSG wakati ikishinda 2-0 huko Troyes na ule wa 5-0 dhidi ya Metz.

Wamarekani wameamua kumuinua mchezaji huyo mwenye  umri wa miaka 23 na siku 84 kwa ajili ya kukutana na nchi hizo, ambazo zimeshindwa kufuzu kwa Kombela Dunia Juni nchini Urusi.

"Mchezo huu kwa mara nyingine tena inawakilishwa na baadhi ya sura mpya, alisema Sarachan. "Sehemu kubwa ya kundi hili ni wachezaji vijana ambao tunafikiri watakuwa na muda mrefu na timu hiyo ya taifa pamoja na wachezaji wengine wazoefu.

Weah ni mmoja kati ya wachezaji watano walioitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha Marekani, pia kinamjumuisha mabeki Antonee Robinson wa Bolton Wanderers, Erik Palmer-Brown wa Ubelgiji.

Wengine ni Bortrijk wa Ubelgiji na Shaq Moore anayeichezea klabu ya Hispania ya Levante pamoja na mshambuliaji Andrija Novakovich wa timu ya Uholanzi ya Telstar.

"Huu ndio muda sasa kuwapatia hawa vijana uzoefu wa mechi za kimataifa, alisema Sarachan. Watapimwa dhidi ya timu yenye uzoefu ya Paraguay."

Palmer-Brown hivi karibuni lisajiliwa na vinara wa Ligi Kuu ya England ya Manchester City na yuko kwa mkopo katika klabu ya Ubelgiji, ambako alianza kuichezea wiki mbili zilizopita.

Mzaliwa wa Uingereza Robinson ameichezea mara 29 timu ya Daraja la Kwanza ya Bolton.

No comments:

Post a Comment