Tuesday 27 March 2018

`Moto Ulioua Watu 64 Uliwashwa kwa Makusudi'


MOSCOW, Urusi
MOTO mkubwa ulioua watu 64, wakiwemo watoto 41, katika kumbi za burudani nchini Urusi, ulisababishwa na `uzembe’,  amesema Rais Vladimir Putin.

Putin aliyasema hayo wakati alipotembelea eneo la tukio huko Kemerovo, Siberia.
Wachunguzi walisema kuwa alamu za moto zilizimwa kwa makusudi, huku milango ya kutokea nje ikifungwa wakati moto huo ulipoanza juzi Jumapili.

Shirika la Habari la Interfax liliripoti kuwa watu kama 300 walikuwa wamejazana nje ya makamu makuu ya serikali ya mitaa wakitaka kuondolewa kwa viongozi wa mamlaka hiyo.

Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana, lakini Kamati ya Uchunguzi imesema kuwa kulikuwa na uvunjifu mkubwa wa taratibu  katika duka hilo kubwa la Winter Cherry mall.

"Nini kilichotokea hapa?",alisema Rais wa Urusi baada ya kuweka shada la maua katika eneo hilo la tukio.
"Watu, watoto walikuja kupumzika, lakini sasa tunazungumzia janga. Tumewapoteza watu wengi kwa sababu gani?...”

Jumapili ilikuwa siku ya mapumziko na watoto wengi walifika hapo na kucheza juu ghorofani bila ya kuwa chini ya uangalizi ya watu wazima, ambao kama wangekuwepo wangeweza kuwasaidia.

Irina alisema katika gho;ofaya pili watu walianza kupiga keleke “Moto moto”. Nilijaribu kurudi nyuma, lakini njia yangu ilizuiwa, watu walikuwa wengi.”

Wazazi wa mtoto aliyekuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa alifanikiwa kuokolewa na marafiki zake. Darina aliungana tena na wenzake katika ghorofa ya kwanza.
Jumba hilo ambalo lilifunguliwa mwaka 2013, lina kumbi nyingi za sinema, migahawa na vituo kadhaa vya bafu za maji ya mvuko.

Baadhi ya maeneo ya jumba hilo kubwa yanadaiwa kuwa kwenye hatari ya kuporomoka.
Moto huo ulianza katika ghorofa ya juu katika jumba Winter Cherry.

Inadaiwa wengi wa waliofariki walikuwa kwenye kumbi za sinema.

No comments:

Post a Comment