Friday 2 March 2018

Lyimo, Anna Waahidi Makubwa TUGHE-JNIA


  Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE), mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Gaudence Kadyango aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), akitoa maelezo kwa wapigaji kura kwenye uchaguzi mdogo wa tawi hilo uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Transit uliopo Jengo la Kwanza la abiria(TBI).


 
Na Mwandishi Wetu
WENYEVITI Bw. Filbert Lyimo na Bi. Anna Myovela wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), wameahidi makubwa katika kutetea haki za wanachama wao mara baada ya kuchaguliwa leo kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika katika ukumbi wa Transit uliopo Jengo la Kwanza la abiria (TBI).

Bw.  Lyimo aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TUGHE tawi la JNIA alisema atahakikisha anawawakilisha vyema wanachama kwa mwajiri, ikiwemo kutetea haki na maslahi yao ya kazi.


    Bw. Filbert Lyimo akijinadi katika nafasi ya Uenyekiti katika  uchaguzi mdogo wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) uliofanyika leo katika ukumbi wa Transit uliopo jengo la kwanza la abiria (TBI).


“Nashukuru kwa kunionesha ushirikiano nyie ndio mlionichagua mimi na sio mimi niliowachagua nyie, hivyo ninaahidi sintawaangusha nitakwenda kifua mbele kutetea haki zenu kwa mwajiri, na jambo la msingi tushirikiane ili kufanikisha haya ninayoyatarajia,” alisema Bw. Lyimo.

Pia amewakumbusha wafanyakazi wote ambao bado kujiunga kwenye chama cha Wafanyakazi sehemu ya Kazi, wafanye hima na wajiunge ili nao wapate haki za kutetewa endapo watapata matatizo mbalimbali.

   Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka (wa kwanza kulia), akifuatilia kwa makini zoezi la uchaguzi mdogo wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la kiwanja hicho uliofanyika leo katika ukumbi wa Transit uliopo jengo la kwanza la abiria (TBI).

Wawakilishi wa wagombea wa nafasi ya Uenyekiti wa Chama  cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), wakihesabu kura leo za nafasi ya Mwenyekiti mara baada ya uchaguzi uliofanyika leo katika Ukumbi wa Transit uliopo jengo la kwanza la abiria (TBI).


Naye Bi. Myovela aliyechaguliwa katika nafasi ya Uenyekiti Kamati ya Wanawake alisema atahakikisha anawatumikia wanachama wote bila kujali umri, dini wala kabila, ambapo amesisitiza hatakuwa na urafiki kwa yeyote  atayekwamisha jitihada zake hizo.
“Naomba ushirikiano wenu mkubwa ili tujenge TUGHE mpya ninayoamini itafanya vizuri kutetea wanachama wote,” alisema Bi. Myovela.  




Hata hivyo katika uchaguzi huo uliokuwa na ushindani  Bw. Lyimo alishinda kwa kishindo kwa kura 39 na kuwashinda Simon Mbogo (32) na Victor Mabote (3).


 Wanachama wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), wakihesabu kura za nafasi ya Uenyekiti Kamati ya Wanawake, katika uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa Transit wa Jengo la Kwanza la abiria (TBI).


Naye Bi. Myovela alipata kura 24 na kuwashinda Rehema Ambari aliyepata kura 17, Mwanahawa Mdee kura moja na Yusta Swebe hakupata kitu.

Kwa upande wa ujumbe Bw. Steven Ntambi alishinda kwa kura tisa, huku mpinzani wake Bi. Ambari akiambulia kura tano.

Uchaguzi huo umefanyika wa kuziba mapengo baada ya aliyekuwa Wenyeviti Bw. Abbas Rweyumamu, na Bi. Simai Ngasani kuhamishwa kituo cha kazi cha JNIA na kupelekwa Makao Makuu, huku Bw. Ntambi akijaza nafasi ya ujumbe iliyoachwa na Lyimo.


  Msimamizi wa uchaguzi mdogo wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bi. Honesta Ngowi kutoka Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana (kulia) akishughudia wanaohesabu kura za nafasi ya ujumbe wa TUGHE katika uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la abiria (TBII).


Hata hivyo kwa nyakazi tofauti wasimamizi wa uchaguzi huo, Katibu Mkuu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Gaudence Kadyango na Bi. Honest Ngowi kutoka Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana waliwataka viongozi waliochaguliwa kuhakikisha wanaongeza idadi ya wanachama ili kuzidisha mshikamano sehemu ya kazi.

Wapiga kura katika uchaguzi mdogo wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), wakimsikiliza Katibu wa tawi hilo, Bw. Thawabu Njeni akitoa ufafanuzi kabla ya kutangazwa kwa matokeo leo kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la abiria (TBII).


Uongozi mzima wa TUGHE-JNIA ni Lyimo (Mwenyekiti), Thawabu Njeni (Katibu), Anna (Mwenyekiti wanawake), Mastidia Ndyomulwango (Katibu Kamati ya Wanawake), Mwanaisha Athuman (Kamati ya Vijana), Kidiga Baltazar (Kamati ya Walemavu), huku wajumbe ni Sadic Milulu, Theobald Beng’inus, Mwanaheri Omar, Adventina Rugimbila, Hussein Msuya, Ntambi na Mbogo.

No comments:

Post a Comment