Tuesday 6 March 2018

Madrid Yatangulia Robo Fainali Mabingwa Ulaya


PARIS, Ufaransa
MABINGWA wa Ulaya Real Madrid imetinga katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kuifunga vinara wa Ligue 1 Paris St-Germain 2-1 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Parc des Princes.

Cristiano Ronaldo ndiye alikuwa kinara wa mchezo huo baada ya kutupia nyavuni moja ya mabao yaliyowezesha timu hiyo ya Hispania kushinda mechi zote mbili, nyumbani na ile ya ugenini.

Mabingwa hao watetezi wametinga robo fainali kwa kupata ushindi wa jumla ya mabao 5-2 baada ya kushinda 3-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika wiki mbili zilizopita Hispania.
Kikosi cha Real Madrid.
Katika mchezo wa kwanza, ambapo walishinda 3-1, Ronaldo alifunga mara mbili huku jingine likiwekwa kimiania na Casemiro katika dakika ya 80.

PSG ilijikuta matatani baada ya kiungo wake, Marco Verratti kutolewa nje baada ya kupewa kadi ya pili ya njano, kabla Edinson Cavani hajafunga bao la machozi.
Kikosi cha PSG
Kwa PSG, ambao ina pointi 14 zaidi kileleni mwa msimamo wa Ligue 1, hii ni msimu wake wa pili mfululizo kutolewa katika hatua ya 16 bora huku ikiacha hatma ya kocha wake Unai Emery kuwa katika utata.

Timu hiyo ilishuka dimbani bila nyota wake majeruhi Mbrazil Neymar na haikusaidiwa na msaada wa Verratti, ambaye alitolewa katika dakika ya 66. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia alitolewa baada ya kumchezea rafu Casemiro katika kipindi cha kwanza na alioneshwa ya pili.

No comments:

Post a Comment