Monday 26 March 2018

Timu Madola Sasa Kuagwa Keshokutwa Jumatano

Mabondia wa timu ya taifa ya Tanzania inayojiandaa kwa Michezo ya Jumuiya ya Madola wakiwa na kocha wao, Moses Oyombi (katikati mbele) baada ya mazoezi yao kwenye ukumbi wa Filbert Bayi Sports Complex Mkuza, Kibaha juzi.

Na Mwandishi Wetu
TIMU ya Tanzania itakayoshiriki Michezo ya 21 ya Jumuiya ya Madola, ambayo ilitarajia kuagwa kesho Jumanne kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, sasa itaagwa keshokutwa Jumatano, imeelezwa.

Habari za uhakika zilizopatikana leo zimesema kuwa timu hiyo haitaagwa kesho kutokana na sababu zisizozuilika na badala yake itaagwa leo na Waziri wa habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.

Tayari Mkuu wa msafara wa timu hiyo, Dk Yussuf Singo, ambaye ni Mkurugenzi wa Michezo nchini, aliondoka jana Jumapili kwenda Gold Coast kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kabla ya kuipokea timu ya Tanzania nchini Australia.

Timu ya riadha itakuwa na Stephano Huche, Said Makula na Sarah Ramadhani (marathon), Failuna Abdul (meta 10,000), Ali Hamisi Gulam (meta 100/200) na Anthony Mwanga (miruko na mitupo) wakati makocha ni Zacharie Barie na Lwiza John.
Mabondia wa timu ya taifa wakianza na kumaliza mazoezi yao kwa sala kila siku.
Ndondi ni Kassim Mbutike (kg 69), Ezra Paulo (kg 56), Haruna Swanga (kg 91) na Seleman Kidunda (kg 75) na kocha wao ni Benjamin Moses.

Timu ya kuogelea inaundwa na Hilal Hilal na Sonia wakati kocha wao ni Khalid Yahya Rushaka.
Nahodha wa timu ya taifa ya mpira wa meza ya Tanzania itakayoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola, Masoud Mtalaso (kulia) akifanyishwa mazoezi na Mkenya Kennedy Kajali katika kambi ya timu hiyo Kibaha mkoani Pwani mwishoni mwa wiki.
Timu ya mpira wa meza inaundwa na Amon Tumaini, Mtalaso, Neema Mwaisyula na Fathiya Pazi wakati kocha wao ni Ramadhan Othman Suleiman.

No comments:

Post a Comment