Tuesday 31 January 2017

Yanga yachomoa kucheza na mabingwa wa Afrika Mamelodi Sundowns nfasi yake yachukuliwa na Azam FC



Na Mwandishi Wetu
YANGA  imekataa kucheza mchezo wa kujipima nguvu na mabingwa wa Afrika, Mamelodi Sundwons ya Afrika Kusini Ijumaa, imeelezwa.

Habari kutoka Yanga, zimesema kuwa kocha wa timu hiyo Mzambia George Lwandamina ndiye aliyegomea mchezo huo akidai kuwa utaingilia program yake ya mazoezi.

Taarifa zaidi zinadai kuwa, Lwandamina amekataa mchezo dhidi ya Mamelodi uliokuwa ufanyike Ijumaa kwa madai kuwa unaingilia mipango yake.

 “Hatutacheza na Mamelodi kwa sababu kocha ameukataa huo mchezo, amesema unaingilia programu zake, kama unavyojua kwa sasa tupo kwenye hatua ngumu ya Ligi Kuu na wakati huo huo tunaingia kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika,”kilisema chanzo chetu.

Baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Mwadui FC, Yanga SC itamenyana na timu nyingine ya Shinyanga ya Stand United Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kwa upande wake, waandaaji wa mechi hiyo pamoja na kusikitishwa na kitendo cha Yanga kugomea mchezo huo, lakini tayari wameiteua Azam FC kuchukua nafasi hiyo.

Sasa Memelodi baada ya kucheza na Simba kesho Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam,  watahamia Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Ijumaa kucheza na Azam.

Timu hiyo inakuja nchini kwa mwaliko wa klabu ya African Lyon ya Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa African Lyon, Rahim Kangenzi ‘Zamuda’ alisema Mamelodi wanakuja nchini kushiriki kampeni ya kupiga vita ujangili, iitwayo Linda Tembo Wetu. 

Na Zamunda amesema timu hiyo  ya mjini Pretoria itakuwa nchini kwa wiki yote ya kwanza Februari kushiriki kampeni hiyo pamoja na kucheza mechi hizo.

Kuhusu kujiondoa kwa Yanga, Zamunda alisema kwamba hawana cha kufanya zaidi ya kukubaliana nao, lakini amesikitishwa na hilo.

No comments:

Post a Comment