Friday 13 January 2017

Vumbi kuanza kutimka kesho Gabon fainali za Mataifa ya Afrika



LIBREVILLE, Gabon
MIAKA, miezi, wiki hatimaye siku zimepita kabla ya kesho Jumamosi kuanza kwa fainali za 31 za Mataifa ya Afrika zitakazofanyika nchini hapa na kushirikisha jumla ya nchi 16 zinazowania taji hilo.

Leo katika ufunguzi wa mashindano hayo kutakuwa na mechi mbili, lakini moja ile itakayoanza saa moja usiku na kuzikutanisha Burkina Faso na Cameroon ndio itakayovuta hisia za wapenzi wengi wa soka.

Mchezo huo umepangwa kuanza saa 4:00 Usiku na kuutangulia ule utakaowakutanisha wenyeji Gabon dhidi ya Guinea-Bissau utakaofanyika kuanzia majira ya saa 1:00 Usiku, ambapo mechi hizo zote za Kundi A, zitapigwa kwenye Uwanja wa Uwanja wa Stade d'Angondjé.

Beki  Bakary Kone, kiingo na nahodha Charles Kabore na mshambuliaji Jonathan Pitroipa kati yao wamecheza mechi 173 na watakuwa wakitegemewa zaidi.

Hatahivyo, Cameroon inashiriki mashindano hayoya Afcon huku ikiwakosa wachezaji wake nane, akiwemo beki wa Liverpool Joel Matip, aliyegomea kuichezea timu ya taifa lake.

Benjamin Moukandjo ndiyer aliyefanywa nahodha mpya kwa Simba hao wasiofungika.

Preview ya Mchezo
Nchi hizo katika historia ya soka la Afrika zimekutana mara moja tu wakati bao la Alphonse Tchami lilipoipatia Cameroon ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Burkina Faso katika mchezo wa ufunguzi wa fainali za mwaka 1998.

Cameroon imeshinda mara nne taji la mashindano hayo, katika miaka ya 1984, 1988, 2000 na 2002, wakati Burkina Faso ilikaribia kabisa kulitwaa taji hilo mwaka 2013 wakati walipomaliza katika nafasi ya pili.

Nchi hizo zote mbili zitatakwa kugangamala na kuimarika zaidi baada ya kushiriki fainali za mwisho mwaka 2015 walipotolewa katika hatua ya makundi. Cameroon walitoka sare mara mbili na kupyeza mchezo mmoja, wakati Burkina Faso ilitoka sare mara moja na kupoteza mara mbili.

Kocha Hugo Broos amemfanya mfungaji wa wakati wote wa Cameroon Lorient scorer Moukandjo kama nahodha wake mpya.

MAKOCHA WANASEMAJE
Kocha wa Cameroon Hugo Broos: "Wakati wote ni muhimu kaunza kwa ushindi. Unaposhinda mchezo wa kwanza unakuwana nafasi ya asilimi 50 ya kuwa na uhakika wa kucheza raundi ya pili.

"Lakini itakuwa ngumu sana kusonga mbele, kwani Burkina Faso miaka michache iliyopita ilicheza fainali za Mataifa ya Afrika na hatutakiwi kuwadharau, kwani ni timu nzuri.”

RATIBA KESHO JUMAMOSI:

Gabon   v          Guinea-Bissau   Stade d'Angondje           1:00  Usiku

Burkina Faso     v          Cameroon         Stade d'Angondje           4:00 Usiku  

Jumapili, Januari 15, 2017

Algeria  v          Zimbabwe         Stade de Franceville    1:00 Usiku
   
Tunisia  v          Senegal            Stade de Franceville      4:00 Usiku
 
Jumatatu, Januari 16, 017

Cote d'Ivoire     v          Togo     Stade d'Oyem   Saa 1:00 Usiku
 
DR Congo         v          Morocco           Stade de Franceville      Saa 4:00 Usiku
 
Jumanne, Januari 17, 2017

Ghana   v          Uganda Stade de Port Gentil      Saa 1:00 Usiku

Mali      v        Misri    Stade de Port Gentil      Saa 4:Usiku
  

No comments:

Post a Comment