Sunday 1 January 2017

Mourinho amtaka Martial kumsikiliza yeye na sio wakala wa mchezaji huyo ili aendelee kuichezea Manchester United



MANCHESTER, England
MSHAMBULIAJI wa Manchester United Anthony Martial anatakiwa "kunisikiliza mimi na sio wakala wake ", anasema kocha wa timu hiyo Jose Mourinho.

Wakala huyo Mfaransa aliripotiwa hivi karibuni akisema kuwa “anaangalia” uwezekano wa mteja wake kuhamia katika klabu ya Sevilla ya Hispania.

Martial,mwenye umri wa miaka 21, alikuwa mfungaji bora wa Man United msimu uliopita baada ya kufunga mabao 17, lakini bao lake la kusawazisha alilofunga jana Jumamosi wakati Manchester United ikiibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Middlesbrough lilikuwa ni bao lake la tano kufunga msimu huu.

"Ni mchezaji wa ajabu na wa aina yake alikuwa mfungaji bora msimu uliopita, “alisema Mourinho.
"Martial alicheza, alitengeneza, pia alifunga. Alipambana, ni mchezaji mzuri. Najua ana kipaji cha hali ya juu sana.”

Martial, aliyejiunga na Man United akitokea Monaco kwa ada ya pauni mioni 36 mwaka 2015, alifanya kazi nzuri wakati timu yake ikitoka nyuma Jumamosi na kuibuka na ushindi huo dhidi ya Boro.

Alisawazisha kwa bao la dakika 85 kabla ya Paul Pogba hajafunga lile la ushindi dakika moja baadae.

Baadae, Mourinho alishauri kuwa Martial anatakiwa kufuata mfano wa mchezaji mwenzake wa timu hiyo Henrikh Mkhitaryan, aliyetakiwa na kocha wake kufanya zaidi, ambapo alijibu kwa kufunga mabao matatu katika mechi nne zilizopita.

Kocha huyo wazamani wa Chelsea aliongeza kusema: "Nilijua Mkhitaryan ni kipaji cha hali ya juu lakini nilikuwa simchezeshi. Kwa kipindi hiki hucheza hata beki ya kushoto wakati timu ikishinda na tunahitaji kulinda ushindi wetu na kuhitaji balansi zaidi.

"Martial anatakiwa kunisikiliza mimi na sio wakala wake. Anatakiwa anisikilize mimi katika mazoezi kila siku na katika kila mrejesho ninaompa kujaribu kumuimarisha na kumboresha zaidi.

"Huku Martial kika kukiha nasoma magazeti,  'Anthony Martial anakwenda Sevilla, Anthony Martial anakwenda kucheza kwa mkopo, Anthony Martial hana furaha'. Anthony Martial anachotakiwa ni kunisikiliza mimi na sio mtu mwingine yeyote.”

Beki wazamani wa United Phil Neville: "Nafikiri ni kitu rahisi. Klabu imewekeza kwa mchezaji huyo kiasi cha pauni milioni 56. Sasa ni jukumu lake kumuuliza wakala wake kwa nini anamuhusisha na kuhamia Sevilla na aseme kwa sasa niko katika moja ya klabu kubwa kabisa duniani. Nataka kuendelea kubaki Man United.”
Nahodha wazamani wa timu ya taifa ya England Alan Shearer: "Martial alikuwa mchezaji bora katika mchezo ule na aliweza kuirejesha Man United mchezoni. Na alicheza vizuri tangu mwanzo wa mchezo.”

No comments:

Post a Comment