Saturday 28 January 2017

Kocha Micho ataka kuiburuza mahakamani Fufa kwa kutomlipa mishahara yake



KAMPALA, Uganda
KOCHA wa timu ya taifa ya Uganda, The Cranes, Milutin 'Micho' Sredojevic (pichani), amelitaka  Shirikisho la Soka la Uganda (Fufa) kutimiza masharti ya mkataba la sivyo atawachukulia hatua za kisheria.

Mserbia huyo, ambaye aliipeleka Uganda Gabon katika mashindano ya Kombela Mataifa ya Afrika (Afcon 2017), kwa mara ya kwanza baada ya kushindwa kufuzu kwa takribani miaka 39, amesema anadai malimbikizo ya mishahara yake.

Micho alisema kuwa wanaweza kulimaliza suala hilo vizuri, lakini kama wakishindwa basi atakimbilia katika vyombo vya kisheria.

Chini ya Micho the Cranes ilitolewa katika hatua ya makundi ya Afcon 2017 nchini Gabon baada ya kufungwa kiduchu na vigogo wa Afrika Ghana na Misri kabla ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Mali.

Kiwango cha timu hiyo ya Uganda kilikuwa kizuri sana na kinaonesha dalili kuwa, timu hiyo imeimarika zaidi, hasa ukilinganisha na timu hiyo iliposhiriki mashindano hayo kwa mara ya mwisho mwaka 1978.

Kocha huyo amekuwa akihusishwa na nchi kibao zikiwemo Ghana – baada ya kocha wa the Back Stars, Avram Grant akijiandaa kuondoka baada ya mashindano hayo ya Mataifa ya Afrika.

"Nina mkataba hadi wakati wa mashindano ya Mataifa ya Afrika mwaka 2019 lakini wakati wote mabeki ya makocha huwa nusu yameshapangwa vitu tayari kubaki na tayari kuondoka,”alisema Micho.

"Uganda inatakiwa kuamua. Kwa kweli niko wazi kwa kila kitu kwa sababu zimekuja ofa nyingi.

No comments:

Post a Comment