Monday 19 June 2017

Wafanyakazi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege waadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma kwa kujadili changamoto wanazokabiliana nazo kazini


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mtengela Hanga wakati akijibu maswali ya wafanyakazi wa mamlaka hiyo leo kwenye ukumbi wa Uwanja wa Ndege wa Terminal One ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma inayomalizika Juni 23. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Ally Mohamed. 
Baadhi ya wafanyakazi wa idara mbalimbali za Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Mastdia akizungumza wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo kwenye Uwanja wa Ndege wa Terminal One.
Wafanyakazi wa Idara mbalimbali za Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) katika mkutano na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wao, Mtengela Hanga (hayuko pichani).
Dickson Elisha wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) akizungumza katika mkutano huo leo.
Musso John akizungumza katika mkutano huo.

No comments:

Post a Comment