Tuesday 20 June 2017

Afungwa baada ya kumning'iniza mtoto ghorofani

ALGIERS, Algeria
MAHAKAMA nchini hapa imemuhukumu kwenda jela miaka miwili mtu mmoja kwa kosa la kumning’iniza mtoto wake nje ya dirisha katika ghorofa refu ili kupata watu wengi katika ukurasa wake wa Facebook.

Mtu huyo alitupia picha yake akiwa ameng’iniza mtoto nje ya dirisha katika jengo refu, huku picha hiyo ikiwa na maelezo (caption):  "Nataka watu 1,000 watakaolaiki (ingia) katika ukurasa wangu wa Facebook au namuangusha chini mtoto huyu.”

Alihukumiwa kwa kosa na kuhatarisha maisha ya mtoto huyo baada ya kukamatwa Jumapili, Polisi ilisema.

Mtoto huyo alining’inizwa katika katika dirisha la ghorofa ya 15 ya makazi iliyopo katika jiji hili, liliripoti shirika la habari la Al Arabiya.

Mtu huyo, mwenye undugu na mtoto huyo, alikanusha shitaka hilo, akisema kuwa picha hiyo ilitengenezwa na watumiaji wa mitandao ya kijamii.

"Picha iliyopigwa ilipigwa katika kibaraza iliyokuwa na vizuizi, Hii ilitolewa na kuwekwa nyingine, “alijitetea.

Baba wa mtoto huyo aliitaka mahakama kumsamehe mtu huyo, akidai kuwa alikuwa akicheza tu.
Hatahivyo, jaji alipinga maombi hayo dhidi ya yake, akisema picha ilikuwa haina utata na ilionesha maisha ya mtoto huyo yalikuwa hatarini.


Watu walichangia katika taarifa hiyo walionesha hasira kuhusu tukio hilo la kinyama.

No comments:

Post a Comment