Sunday 25 June 2017

Serikali waipa TOC hekali 20 za ardhi Singida



Mkuu wa Mkoa wa Singida, Rehema Nchimbi akiwa na atoto walioshiriki mbio za kilometa 2,5 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Olimpiki Duniani ambayo kitaifa ilifanyika Singida leo kwenye Uwanja wa Peoples.
 Na Mwandishi Wetu, Singida
SERIKALI ya Mkoa wa Singida imetoa ardhi  hekali 20 kwa Kamati ya Ollimiki Tanzania (TOC) kwa ajili ya kujenga kituo cha michezo cha Olimpiki Afrika.

Watoto wakishiriki mbio za kilometa 2.5 wakati wa Siku ya Olimpiki iliyofanyika kitaifa mkoani Singida leo kwenye Uwanja wa Peoples mjini humo.

Nchimbi alitoa ahadi hiyo jana wakati wa maadhimisho ya Siku ya Olimpiki iliyofanyika kitaifa mkoani hapa kwenye Uwanja wa Peoples hapa, ambako washiriki walianza mbio na kumalizia kwenye uwanja huo.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania TOC), Filbert Bayi akizungumza na wana habari baada ya kumalizika kwa maazimisho ya Siku ya Olimpiki kwenye Uwanja wa Peoples mjini Singida.

Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi alimshukuru Nchimbi na kusema kuwa ofa hiyo ataiwakilisha kwa wenzake akiwemo rais wa kamati hiyo, Gulam Rashid na Kamati ya Utendaji ili kuona wanaipokeaje ofa hiyo.
Katika hafla hiyo mtoto wakike na kiume wenye umri mdogo na mwanamke na mwanaume mwenye umri mkubwa zaidi, kila mmoja alizawadiwa zawadi na Nchimbi iliyotolewa na TOC.
  Mkuu wa Mkoa wa Singida, Rehema Nchinbi akicheza ngome ya Kinyaturu ya Misake. Kulia ni Katibu tawala, Angelina Lutambi. 

Kwa upande wa watoto wenye umri mdogo zaidi waliomaliza wa kwanza katika mbio zao za kilometa 2.5, Careen Msasu mwenye umri wa miaka sita na Stephen Joshua mwenye umri wa miaka 8 ndio walitwaa sh 50,000 kila mmoja kwa kumaliza wa kwanza.

 Bibi wa zaidi ya miaka 90 akipokea zaadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Rehema Nchimbi baada ya kumaliza na mbio na watoto wadogo.

Kwa upande wa watu wenye umri mkubwa zaidi walioshiriki mbio hizo, Vitus Mutake mwenye miaka 71 na Tatu Chungu mwenye umri wa miaka 59, nao walitwaa sh 50,000 kwa kumaliza wa kwanza huku wakiwa wenye umri mkubwa kuliko washiriki wengine wa mbio za kilometa tano.

Siku ya Olimpiki duniani imekuwa ikifanyika Juni kila mwaka na kuadhimishwa na zaidi ya nchi 200 duniani, ambazo ni wanachama wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC).

Siku ya Olimpiki mjini hapa ilianza kuadhimishwa juzi kwa usafi wa mazingira ambao Nchimbi na viongozi wa TOC walisafisha mazingira katika mitaa na maeneo mbalimbali ikiwemo shule ya msingi Mwenge na soko la matunda.










No comments:

Post a Comment