Saturday 24 June 2017

RC Singida, TOC waendesha zoezi la usafi leo


Mkuu wa  Mkoa wa  Singida, Rehema Nchimbi (watatu kulia), Katibu Mkuu wa  Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi (wapili kulia) na mjumbe wa Kamati ya Utendaji Irine Mwasanga wakati wa kufanya usafi mjini Singida leo sambamba na maadhimisho ya Siku ya Olimpiki inayofanyika kesho.
Na Mwandishi Wetu, Singida
WAKATI maadhimisho ya Siku ya Olimpiki Duniani yanafanyika kitaifa kesho mjini Singida, Mkuu wa Mkoa huo pamoja na viongozi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), leo walifanya usafi katika maeneo mbalimbali.

MKUU wa Mkoa wa Singida, Rehema Nchimbi pamoja na viongozi mbalimbali wa TOC walifanya usafi katika maeneo tofauti tofauti ili kuadhimisha Siku ya Olimpiki ambayo itafanyika kesho Jumapili.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Rehema Mchimbi (katikati) akishiriki katika usafi mjini Singida leo. Kushoto ni Makamu wa Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Henry Tandau. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida (RPC),   
Akizungumzia kuhusu Siku ya Olimpiki, Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi alisema kuwa, Nchimbi ndiye atabariki maadhimisho ya Siku ya Olimpiki kwenye Uwanja wa People uliopo mjini Singida.

Bayi alisema kuwa wanafunzi shule mbalimbali za msingi na sekondari pamoja na watu wengine, watashiriki mbio hizo za kilometa 2.5 pamoja na zile za wakubwa, ambazo zitakuwa za kilometa tano.

Maadhimisho hayo ya Siku ya Olimpiki yatashuhudia washiriki wakikimbia katika mbio hizo, ambayo hayana ushindi lakini mshiriki mwenye  umri mdogo na yule mwenye umri mkubwa zaidi, ndio watakaokabidhiwa zawadi za ushindi.


Maadhimisho ya Siku ya Olimpiki Duniani yamekuwa yakifanyika Juni kila maka , ambapo mwaka jana yalifanyika mjini Mtwara na mgemi rasmi alikuwa mkuu wa mkoa huo, Halima Dendegu na kuwashirikisha wakuu wote wa wilaya za mkoa huo.











No comments:

Post a Comment